WAKULIMA MKOANI DODOMA WASHAURIWA KULIMA MAZAO YANAYOHIMILI UKAME

WAKULIMA MKOANI DODOMA WASHAURIWA KULIMA MAZAO YANAYOHIMILI UKAME

Na Hamida Ramadhani-Dodoma KATIKA kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi wakulima wa Mkoa wa Dodoma wameshauriwa kuendelea kulima mazao yanayostahimili ukame  ikiwemo  zao la Mtama na Uwele. Wito huo umetolewa jiji hapa na Meneja Mradi wa Kilimo   hifadhi kutoka Dayosisi ya Central Tanganyika DCT Busela Yuga alipotembelewa kwenye Bada lao la Kilimo

Na Hamida Ramadhani-Dodoma


KATIKA kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi wakulima wa Mkoa wa Dodoma wameshauriwa kuendelea kulima mazao yanayostahimili ukame  ikiwemo  zao la Mtama na Uwele.

Wito huo umetolewa jiji hapa na Meneja Mradi wa Kilimo   hifadhi kutoka Dayosisi ya Central Tanganyika DCT Busela Yuga alipotembelewa kwenye Bada lao la Kilimo katika wiki ya Mazingira inayoendelea viwanja vya JK Jijini Dodoma 


Meneja huyo amesema kuwa,kama iliyoelezwa na Waziri Mkuu Kassim  Majaliwa Kassim kwamba ripoti ya tatu ya hali ya Mazingira iliyofanya mwaka 2019 imeonyesha Mkoa wa Dodoma umeathiliwa kwa hekta 373,000 kwa shughuli za ukataji miti na misitu kwaajili ya matumizi ya Kuni na mkaa.
” Kuathiriwa huko kwa kiasi kikubwa katika Mkoa wa Dodoma kumepelekea Dodoma kuonekana kame na jangwa na ndio Maana Sisi kama wataalamu wa Kilimo tunaendelea kuwaelimidha wananchi na jamii  kulima mazao yenyekustahimili ukame Ili wawe na Uhakika wachakula nadani ya kaya,” amesema Yuga.

Aidha amesema pia wameendelea kutoa elimu ya upandaji kwa wakulima huku wakiwahamasisha wakulima kupanda mazao yanayastahimili ukame ilikukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.


“Tunawashauli wananchi wa mkoa wa Dodoma kupanda mazao yanayostahimili ukame kama vile  mtama na Uwele pia wapande mazao jamii ya mikunde kama vile Mkunaa ,Canavalia,fiwi kwani mazao hayo yamekuwa yanaifadhi maji na kurutubisha udogo,.
“Takwimu zinaonyesha endapo utafuata utaratibu huo wa kupanda mimea jamii ya mikunde inamfanya Mkulima kulima mavuno kwa wingi.
” Takwimu zinaonyesha mtu akipanda mazao ya mikunde kwenye shamba lake alilolima uele na Mtama Mkulima huyo anaweza kuvuna magunia Saba hadi 12 kwa shamba la kekta moja,” ameeleza Meneja huyo.

Hata hivyo amesema  mradi huo wa Kilimo hifadhi wenye lengo la kuwafanya wananchi na wakulima kuwa na uhakika wa chakula ndani ya kaya ni mradi wa miaka mita na upo katika Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Dodoma mjini,Bahi na Chamwino.

Naye Yusuph Malenda  mkulima wa zao la Mtama katika kijiji cha Nghumbi amesema wamepatiwa elimu ya upandaji na Mbegu bora kwa kuzingatia utaratibu maalumu.

Malenda amesema    shamba lake lina ukubwa wa hekari 2 ambapo anategemea kuvuna kilogram 200 za Mtama ambapo ataweza kuwauzia wakulima wenzake 100  kwa shilingi 3000.

“Zao la Mtama ndio  zao mtambuka kwa kijiji cha Nghumbi kwani mimi ni mmoja wa wakulima wa mfano niliye lima kwa Mbegu bora na manufaa yake ndio kama Haya yanayoonekana,”amesema Mkulima Malenda.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »