Na Barnabas Kisengi-Dodoma KATIKA kuhakikisha ulinzi na usalama kwa wazee wote hapa nchini unaimarika, serikali inaratibu utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kutokomeza mauaji ya wazee 2018/ 2019 – 2022- 2023, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ulinzi na usalama wa wazee wasiojiweza na ambao hawana watu wa kuwatunza huku serikali ikiendelea kusimamia matunzo katika makazi
Na Barnabas Kisengi-Dodoma
KATIKA kuhakikisha ulinzi na usalama kwa wazee wote hapa nchini unaimarika, serikali inaratibu utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kutokomeza mauaji ya wazee 2018/ 2019 – 2022- 2023, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ulinzi na usalama wa wazee wasiojiweza na ambao hawana watu wa kuwatunza huku serikali ikiendelea kusimamia matunzo katika makazi ya wazee.
Akitoa tamko kwa Waandishi wa Habari,Leo Jijini Dodoma kuelekea siku ya Kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wazee ,Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto Dkt, Doroth Gwajima amesema Serikali imeendelea kuzitambua familia masikini wakiwemo wazee na kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi.
Amesema kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inatambua haki ya msingi ya kuishi ambapo inasema kila mtu anahaki ya kuishi na kpata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake kwamujibu wa sheria Ibara ya 16 ya katiba inayotambua haki ya ulinzi wa nafsi yake
Aidha ametoa rai kwa wale wote ambao wamekuwa wakiwaza kuendelea kufanya vitendo vya ukatili kwa wazee ikiwemo ukatili wa kimwili, kihisia na kiuchumi wajue kuwa mkono wa sheria ni mrefu na sheria itachukua mkondo wake kikamilifu pindi wakibainika wamefanya vitendo hivyo
Kaulimbiu ya siku ya Kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wazee inasema ‘’tupaze sauti kupinga ukatili dhidi ya wazee’’
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *