Wizara ya Kilimo imepitisha mbinu ya kukuza uwekezaji .

Wizara ya Kilimo imepitisha mbinu ya kukuza uwekezaji .

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imepitisha mbinu ya kukuza uwekezaji unaolengwa kuelekea mnyororo wa maalum wa thamani hususani katika kuboresha uzalishaji. Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda ameyasema hayo tarehe 11 Juni 2021 wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wawekezaji wa Ulaya katika jukwaa la kilimo. Amesema kuwa uzalishaji mdogo wa mazao umekuwa tatizo kubwa

Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wawekezaji katika sekta ya Kilimo kutoka bara la Ulaya, tarehe 11 Juni 2021 Jijini Arusha. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo).
Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda akichangia mada wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wawekezaji katika sekta ya Kilimo kutoka bara la Ulaya, tarehe 11 Juni 2021 Jijini Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa jukwaa la kilimo la wawekezaji wa bara la Ulaya Bi Cikay Richard akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wawekezaji katika sekta ya Kilimo kutoka bara la Ulaya, tarehe 11 Juni 2021 Jijini Arusha.
Sehemu ya wawekezaji wa walioshiriki katika Mkutano wa wawekezaji katika sekta ya Kilimo kutoka bara la Ulaya, tarehe 11 Juni 2021 Jijini Arusha wakifuatilia kwa makini mjadala kuhusu mazao ya mboga na matunda.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wafanyabiashara wa Mbegu Tanzania (TASTA) Ndg Bob Shuma akifuatilia kwa makini Mkutano wa wawekezaji katika sekta ya Kilimo kutoka bara la Ulaya, tarehe 11 Juni 2021 Jijini Arusha.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imepitisha mbinu ya kukuza uwekezaji unaolengwa kuelekea mnyororo wa maalum wa thamani hususani katika kuboresha uzalishaji.

Waziri wa Kilimo Mhe Prof. Adolf Mkenda ameyasema hayo tarehe 11 Juni 2021 wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wawekezaji wa Ulaya katika jukwaa la kilimo.

Amesema kuwa uzalishaji mdogo wa mazao umekuwa tatizo kubwa kwa wakulima nchini, ingawa tayari serikali imeboresha upatikanaji wa pembejeo ikiwemo mbegu, mbolea pamoja na viuatilifu.

Waziri Mkenda amesema kuwa serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo Awamu ya II (ASDP II) kwa kipindi cha mwaka 2017-2020 imeondoa/kufuta ada takribani 105, na tozo ambazo zilitozwa na bodi mbalimbali za mazao na taasisi za kilimo.

“Pia tumechukua hatua kadhaa kurekebisha Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, 1982 kupitia Sheria ya Fedha, 2017 ambayo inapunguza mazao kuanzia asilimia 5 hadi 3 ili kupunguza gharama za kufanya biashara kwa wawekezaji katika sekta ya kilimo” Amekaririwa Prof Mkenda

Pia Waziri Mkenda amesema kuwa ili kuimarisha sekta ya kilimo nchini serikali imepunguza ada ya upimaji wa mbolea wakati wa usajili. Ada ya upimaji ilikuwa ya juu kama USD ya 300,000 na waombaji walihitaji msimu wa tatu (3) kuthibitisha ufanisi wake ambapo ada hiyo ya upimaji imepunguzwa hadi kufikia 100,000

Prof Mkenda amesema kuwa lengo la kupunguza ada hiyo ni kufanya kilimo kuwa na ustahimilivu, jumuishi, yenye ufanisi na mwitikio wa soko kote nchini.

Amesema kuwa chini ya ASDP II, Wizara ya Kilimo inashirikisha wadau wote ikiwa ni pamoja na sekta binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau wa maendeleo katika maeneo mbalimbali kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa hadi taifa hadi ili kuwezesha mbinu itakayopelekea kuwa na maendeleo endelevu ya kilimo.

Amesema kuwa ASDP II inakuwa sehemu ya mnyororo wa maendeleo ya sekta ya kilimo kwa kuunganisha malengo ya CAADP na kuakisi zaidi maono na kanuni zinazoendana na maelekezo ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi, FYDP na hotuba yenye maono ya Tanzania endelevu iliyotolewa Bungeni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya mboga na matunda-TAHA Dkt Jacqueline Mkindi amesema kuwa mkutano huo umekuwa ni fursa kubwa ya kuwaweka karibu na serikali wawekezaji wa sekta ya mboga na matunda kwani watatumika kama chachu ya kuwaalika wawekezaji wengine kuja nchini.

Amesema kuwa wawekezaji wote nchini wana furaha kubwa kutokana na serikali kuyaeleza kwa ufanisi ikiwemo kuondoa mambo karibu nane kwenye bajeti yam waka 2021/2022 yahusuyo ushuru pamoja tozo ambazo hazikuwa rafiki katika sekta hiyo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa jukwaa la kilimo la wawekezaji wa bara la Ulaya Bi Cikay Richard ameeleza kuwa mkutano huo umewakutanisha wawekezaji wa Kilimo kutoka bara la Ulaya ambao kwa kiasi kikubwa wameeleza changamoto ambazo zinawakabili hususani katika sekta ya mboga na matunda (Horticulture).

Ameongeza kuwa mjadala mkubwa zaidi katika mkutano huo umejikita katika kutafakari kwa pamoja namna ya kuimarisha sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuwa na faida ya jumla kwa wawekezaji lakini kuimarisha pato la kigeni kwa serikali.

Kadhalika, Mkurugenzi wa kampuni ya Hortanzia Afrika Sun Fruit Bw Rory Nightingale na Mkurugenzi wa Kampuni ya YYTZ Bw Fahad Awadh wameipongeza serikali kwa dhamira yake ya dhati kukutana na wawekezaji ili kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili.

Na Mwandishi wetu-Arusha.

June 11 2021.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »