Rais Samia Suluhu Hassan, amesema wakati mwingine dini na siasa vinakinzana.

Rais Samia Suluhu Hassan, amesema wakati mwingine dini na siasa vinakinzana.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa wakati mwingine dini na siasa vinaendana lakini pia wakati mwingine ni vitu vivyokinzana ambapo amesisitiza kwamba vyote hivyo vinatakiwa kutazamwa kwa umakini. Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Julai 8, 2021, mkoani Morogoro aliposhiriki Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT),

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa dini alipowasili katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo (CCT) Kilakala, Mkoani Morogoro.
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Serikali alipowasili katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo (CCT) Kilakala, Mkoani Morogoro.
Baadhi ya viongozi wa dini na Wakristo waliohudhuria katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo (CCT), Kilakala Mkoani Morogoro.
Rais Samia akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili mkoani humo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa wakati mwingine dini na siasa vinaendana lakini pia wakati mwingine ni vitu vivyokinzana ambapo amesisitiza kwamba vyote hivyo vinatakiwa kutazamwa kwa umakini.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Julai 8, 2021, mkoani Morogoro aliposhiriki Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili mkoani humo aliyoianza hapo jana akitokea Jijini Dodoma.

Rais Samia pia amezitaka taasisi za kidini zinazotoa huduma ya kielimu na afya kuweka uwazi katika utendaji wa kazi zao ikiwemo ukaguzi wa hesabu ili kutoa fulsa kwa maafisa wanaotoza kodi kuweka utaratibu mzuri.

Kwa upande wake mwenyekiti wa jumuiya ya kikristo Tanzania Askofu Dkt Alinisa Cheyo amesema kuwa pamoja na mambo mengine makanisa yanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa vibali vya kazi hasa kwa raia wa kigeni ambao wanakuja kutoa huduma katika taasisi za afya na elimu.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »