SERIKALI YAWAONYA WANAOPANDISHA BEI YA GESI KIHOLELA

SERIKALI YAWAONYA WANAOPANDISHA BEI YA GESI KIHOLELA

SERIKALI imetoa onyo kwa wafanyabiashara wa gesi wanaouza na kupandisha bei  gesi  kiholela na kuwaumiza wananchi Waziri wa nishati Medard Kaleman ametoa onyo hilo jijini Dodoma mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya nishati ikiwemo kituo cha Mtambo wa kufua na kupozea umeme kilichopo Zuzu pamoja naku kuwatembelea wasambazaji na wauzaji

SERIKALI imetoa onyo kwa wafanyabiashara wa gesi wanaouza na kupandisha bei  gesi  kiholela na kuwaumiza wananchi

Waziri wa nishati Medard Kaleman ametoa onyo hilo jijini Dodoma mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya nishati ikiwemo kituo cha Mtambo wa kufua na kupozea umeme kilichopo Zuzu pamoja naku kuwatembelea wasambazaji na wauzaji wa gesi.

Waziri kaleman amesema ni lazima tamko la serikali lizingatiwe ambapo mtungi wa gesi wenye kilo 6  unatakiwa kuuzwa chini ya Tsh.elfu ishirini na mbili[22,000] na mtungi wa kilo 15 inatakiwa kuuzwa chini ya  elfu hamsini na tatu[53,000]

  Hivyo.Waziri Kaleman ametoa maelekezo kwa  Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati naMaji (EWURA] kuendelea kufanya mtazamo zaidi ili bei za gesi kushuka zaidi badala ya kupanda

Hatua hiyo imekuja baada ya malalamiko ya wananchi kuongezeka kutokana na bidhaa hiyo muhimu ya nishati kuanza kupanda kila kukicha hali iliyopelekea wananchi kuanza kutoa malalamiko ambapo pia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati naMaji (EWURA] imeshatoa maelekezo juu ya bei elekezi ya gesi.

Na Barnabas Kisengi, Dodoma

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »