“NITAENDELEA KUWAAMINI WANAWAKE KWA KUWAPA NAFASI ZA UONGOZI”.Rais Dkt. Mwinyi.

“NITAENDELEA KUWAAMINI WANAWAKE KWA KUWAPA NAFASI ZA UONGOZI”.Rais Dkt. Mwinyi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Hussein Ali Mwinyi amekipongeza Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) kwa jitihada zao katika kuandaa viongozi bora wanawake wanaotoa mchango kwa maendeleo ya Taifa. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameleza hayo kupitia Hotuba alioisoma kwa niaba ya Rais

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla .


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Hussein Ali Mwinyi amekipongeza Chama cha Wahasibu Wanawake Tanzania (TAWCA) kwa jitihada zao katika kuandaa viongozi bora wanawake wanaotoa mchango kwa maendeleo ya Taifa.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameleza hayo kupitia Hotuba alioisoma kwa niaba ya Rais Dk. Huseein Mwinyi katika ufunguzi wa kongamano la nne la uongozi la wanawake wahasibu Tanzania (TAWCA) lililofanyika katika ukumbi wa Hotel Verde Mtoni Jijini Zanzibar.

Mhe. Hemed amesema amefurahishwa na mikakati iliowekwa na chama hicho katika kuhakikisha wanalisaidia taifa kwa kuandaa viongozi mbali mbali wanawake ambao wamekuwa wakitoa mchango wao katika kukuza Uchumi wa Nchi.


Makamu wa Pili wa Rais amesema kwamba Tanzania ina viongozi wengi wakupigiwa mfano ambao wameweza kushika nafasi mbali mbali kitaifa na kimataifa, kutokana na uwezo walionao wao. jambo ambalo limetoa Imani kubwa kwa jamii kwa viongozi wanawake.


Pamoja na mambo mengine Makamu wa Pili wa Rais amewataka washiriki hao kuunga mkono jitihada zinazochukuliwa na Serikali zote mbili katika  kupiga vita rushwa pamoja na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za umma.


Nae, Mwenyekti wa Chama cha Wahasibu Wanawke Tanzania Dk. Neema Kiure Msussa, ameleza kuwa Chama hicho kimesajiliwa mwaka 2015 ambapo hadi sasa kina jumla ya wanachama 730.


Alieleza kuwa, TAWCA  katika kuwawezesha wajasirimali wanawake imesaidia jumla ya wanawake 101 kwa kuwapatia elimu pamoja na kuwapa mafunzo na mitaji kwa ajili ya kuimarisha harakati zao za kimaisha kupitia biashara.


Akiwasilisha salamu kutoka Hospitali ya Agakhan katika kongamano hilo Dk. Erine Kitege alieleza kuwa katika Kongamano hilo wataalamu kutoka Hospital hiyo watafanya vipimo vya saratani ya Shingo ya kizazi na saratani ya matiti kutokana na kina mama kukumbwa na ugonjwa huo. Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR)Agosti 19, 2021.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »