Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango na Mkewe Mama Mbonimpawe Mpango wameshiriki ibada ya kumuaga marehemu Padre Paul Haule aliyekuwa Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Petro Osterbay Jijini Dar es salaam. Marehemu Padre Paul Haule pia alikuwa Mkurugenzi wa Vyombo vya Habari vya Tumaini vinavyomilikiwa na Kanisa katoliki hapa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango na Mkewe Mama Mbonimpawe Mpango wameshiriki ibada ya kumuaga marehemu Padre Paul Haule aliyekuwa Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Petro Osterbay Jijini Dar es salaam. Marehemu Padre Paul Haule pia alikuwa Mkurugenzi wa Vyombo vya Habari vya Tumaini vinavyomilikiwa na Kanisa katoliki hapa nchini.
Mara baada ya ibada ya kumuaga Padri Haule, Akitoa salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais amemtaja marehemu padre Haule kuwa mtu aliependa kuhubiri Amani na wakati wote alikua mpole na mnyenyekevu.
Amesema Kanisa limempoteza padre aliyekuwa mvumilivu wakati wote na amewaomba waumini kuendelea kumuombea marehemu Padre Haule ili apumzike kwa amani.
Katika hatua nyingine Makamu wa Rais amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Corona. Aidha amewaasa waumini kuendelea kuwakinga viongozi wa dini dhidi ya ugonjwa huo hasa katika wakati wanapokutana kupokea huduma kutoka kwa viongozi hao. Amesisitiza Viongozi wa dini pamoja na waumini kuvaa barakoa wakati wote wanapokuwa katika ibada na katika maombezi mbalimbali yanayofanyika hususani kwa wagonjwa.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *