WAZIRI GWAJIMA ASEMA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BADO CHANGAMOTO SEKTA YA AFYA

WAZIRI GWAJIMA ASEMA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BADO CHANGAMOTO SEKTA YA AFYA

Na Barnabas Kisengi,Dodoma  Waziri wa Afya Mendeleo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto DKt  Dorothy Gwajima amesema kuwa matumizi ya takwimu zenye ubora katika ngazi za chini ili kuweza kufanya maamuzi ya kisayansi bado ni changamoto katika halmashauri nchini jambo ambalo linarudisha nyuma Sekta ya Afya. Akizungumza  kwenye madhimisho ya siku ya Epidemiology Duniani  leo jijini Dooma katika

Na Barnabas Kisengi,Dodoma 

Waziri wa Afya Mendeleo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto DKt  Dorothy Gwajima amesema kuwa matumizi ya takwimu zenye ubora katika ngazi za chini ili kuweza kufanya maamuzi ya kisayansi bado ni changamoto katika halmashauri nchini jambo ambalo linarudisha nyuma Sekta ya Afya.

Akizungumza  kwenye madhimisho ya siku ya Epidemiology Duniani  leo jijini Dooma katika viwanja vya Nyerere Square  waziri huyo amesema kuwa ili kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa na matukio yanayoathiri afya ili kutambua mapema viashiria hatari kwa jamii lazma pawepo na takwimu zenye ubora katika ngazi ya halmahauri.

Aidha waziri Gwajima ameeleza kuwa jumla ya watumishi mia tano kumi na mbili kutoka idara ya afya ya binadamu na idara ya afya ya  mifugo wamepatiwa mafunzo katika ngazi ya kozi ya awali kutoka mikoa yote 26 na halmashauri mia moja hamsini na tisa kwa kipindi cha miaka sita.

 kwa upande wake Rais wa Chama cha Wataalamu wa Epidemology na maabara Tanzania  Dkt. Elibariki Mwakapeje (Tanflea) amesema kuwa wao kama Tanflea ni kuhakikisha afya ya  mtanzania inaimarika ili watu waweze kuwa na afya bora ili aendelee kufanya shughuli zao za kila siku.

Madhimisho haya ya siku ya Epidemiology  yamefanyia kwa mara ya kwanza nchini Tanzania .

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »