Mheshimiwa Spika, leo hii tunafikia tamati ya Mkutano wa Nne wa Bunge la 12 laJamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioanza kikao chake cha kwanza tarehe 31 Agosti, Hivyo, hatunabudi kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwakutuwezesha kuhitimisha shughuli zote zilizopangwa kwenye mkutano huu tukiwa buheriwa afya. Mheshimiwa Spika, vilevile, ninakushukuru wewe binafsi kwa kumudu kuliongozavema
Mheshimiwa Spika, leo hii tunafikia tamati ya Mkutano wa Nne wa Bunge la 12 la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioanza kikao chake cha kwanza tarehe 31 Agosti,
Hivyo, hatunabudi kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa
kutuwezesha kuhitimisha shughuli zote zilizopangwa kwenye mkutano huu tukiwa buheri
wa afya.
Mheshimiwa Spika, vilevile, ninakushukuru wewe binafsi kwa kumudu kuliongoza
vema Bunge hili tukufu, ukisaidiwa na Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa
Wenyeviti wa Bunge. Aidha, niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa michango
mizuri mliyoitoa kwa kusema na kwa maandishi wakati wa kuchangia hoja mbalimbali
zilizowasilishwa na Serikali kwenye mkutano huu.
Mheshimiwa Spika, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wenzangu
kuwa, Serikali kwa upande wake ipo tayari muda wote kupokea michango yenu yenye lengo
la kusaidia kuboresha utekelezaji wa mipango yake.
Salamu za Pole
Mheshimiwa Spika, niungane na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kukupa pole
kufuatia taarifa za kuhuzunisha za kifo cha Mheshimiwa Elias John Kwandikwa aliyekuwa
Mbunge wa Ushetu na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kilichotokea tarehe 2
Agosti, 2021. Aidha, natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na
wananchi wote wa Jimbo la Ushetu kwa kuondokewa na mwakilishi wao huyo.
Mheshimiwa Spika, vilevile, natoa salamu za pole kwa Kamanda Simon Nyakoro
Siro, Inspekta Jenerali wa Polisi kufuatia tukio lililotokea tarehe 25 Agosti, 2021 jijini Dar es
Salaam, ambapo askari wetu wazalendo wapatao watatu na mlinzi mmoja wa kampuni
binafsi waliuawa wakati wakitekeleza majukumu yao ya kiusalama. Mwenyezi Mungu azilaze
roho za marehemu mahala pema na awape uponyaji wa haraka majeruhi wa tukio hilo.
Amin!
Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kuwapa pole Watanzania wenzangu
waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki na wengine kupata ulemavu katika matukio
mbalimbali ikiwemo ajali za barabarani zilizogharimu maisha ya maafisa watano wa
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), waliofariki dunia tarehe 23 Agosti, 2021 wakati
wakitekeleza majukumu yao ya kikazi mkoani Songwe. Mwenyezi Mungu aziweke roho za
marehemu mahala pema peponi. Amina!
SHUGHULI ZA BUNGE
Maswali na Majibu
Mheshimiwa Spika, wakati wa mkutano huu wa 4 wa Bunge la 12, Waheshimiwa
Wabunge wamepata fursa ya kuuliza maswali ya msingi 119 na maswali 263 ya nyongeza ambayo yalijibiwa na Serikali. Kadhalika, maswali 14 ya papo kwa papo yaliulizwa na
Waheshimiwa Wabunge na kujibiwa na Waziri Mkuu.
Maazimio ya Bunge
- Mheshimiwa Spika, vilevile, Waheshimiwa Wabunge walijadili na kupitisha
maazimio mawili ya Bunge kama ifuatavyo: –
Moja: Azimio la Bunge kuhusu kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya
Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula (East African
Community Protocol on Sanitary and Phytosanitary – SPS Measures);
Mbili: Azimio la Bunge kuhusu kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika (African Continental Free Trade Area – AfCFTA); na
- Mheshimiwa Spika, kuridhiwa kwa maazimio haya kutasaidia nchi yetu kuimarisha
biashara na uwekezaji kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki sambamba na kuongeza
shughuli za biashara na uwekezaji wa ndani baina ya nchi wanachama wa Umoja wa Afrika.
Halikadhalika, kutaiwezesha Tanzania kuimarisha ushirikiano na mataifa mengine
wanachama wa Umoja wa Afrika.
Miswada ya Sheria - Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge pia, walijadili na kupitisha miswada
mitano ya sheria iliyowasilishwa na Serikali katika mkutano huu kama ifuatavyo: –
Moja: Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.2 wa Mwaka 2021;
Mbili: Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.4 wa Mwaka 2021;
Tatu: Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Usajili wa Wahasibu na
Wakaguzi wa Hesabu wa Mwaka 2021;
Nne: Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
wa Mwaka 2021. Marekebisho haya pia yanakusudia kuhakikisha shughuli za
zimamoto na uokoaji nchini zinafanyika kwa ufanisi ili kuendelea kuwavutia
wawekezaji kwa kuwahakikishia usalama wa maisha na mali zao; na
Tano: Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.5 wa Mwaka 2021.
- Mheshimiwa Spika, nirejee tena kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa
michango yao mizuri iliyotolewa wakati wa kujadili Miswada hiyo muhimu ambayo itasaidia
kuondoa mapungufu yaliyobainika sambamba na kuboresha baadhi ya masharti katika
utekelezaji wa sheria hizo. Serikali itafanyia kazi maoni na ushauri uliotolewa kwa lengo la
kuhakikisha utekelezaji wa sheria hizo unawanufaisha Watanzania. - Mheshimiwa Spika, niwapongeze na kuwashukuru Waheshimiwa Mawaziri na
Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri ya kuwasilisha Miswada iliyojadiliwa katika mkutano huu
pamoja na kutoa ufafanuzi mbalimbali wakati wa kujibu hoja za Waheshimiwa Wabunge.
Aidha, nimpongeze Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na wataalamu wake kwa kazi
nzuri ya kuandaa miswada iliyowasilishwa katika mkutano huu. - MAENEO YA MSISITIZO KISEKTA
- Mheshimiwa Spika, jukumu langu la msingi lililonisimamisha mbele ya Bunge lako
tukufu ni kutoa maelezo mafupi hususan kuhusu shughuli za mkutano huu wa nne wa
Bunge kabla ya kuahirishwa. Hata hivyo, kabla ya kuhitimisha mkutano huu naomba niweke
msisitizo wa baadhi ya masuala kwa viongozi, watendaji na wananchi kwa ujumla katika
kutekeleza majukumu yao ya kuwaletea maendeleo. - Mheshimiwa Spika, baadhi ya maeneo ambayo nitayatolea msisitizo ni suala la
tozo na uendelezaji wa miundombinu ya afya ya msingi, maandalizi ya uandikishaji wa
wanafunzi wa kidato cha kwanza Januari 2022, matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani,
ujenzi wa Mji wa Serikali, tahadhari dhidi ya UVIKO-19 na michezo.
UENDELEZAJI WA MIUNDOMBINU YA AFYA YA MSINGI - Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Sera ya Afya ya Mwaka 2007 yenye lengo
la kuwashirikisha wananchi katika ujenzi wa vituo vya afya na zahanati. Azma ya Serikali ni
kuona kila kata inapata kituo cha afya na kila kijiji kinakuwa na zahanati ili kusogeza
huduma hizo karibu na wananchi na kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu. Hadi sasa,
tarafa 363 zilizopo Tanzania Bara zina vituo vya afya vyenye uwezo wa kutoa huduma za
upasuaji za dharura, huduma za mionzi na maabara za kisasa. - Mheshimiwa Spika, ili kuzifikia tarafa nyingi zaidi, Serikali imeamua, kwanza
kuzitambua kata za kimkakati na tarafa zote ambazo hazina vituo vya afya. Pili, kutumia
fedha zitokanazo na tozo za miamala ya simu kujenga vituo vya afya vya kimkakati
ambavyo vitakuwa na uwezo wa kutoa huduma za upasuaji za dharura, huduma za mionzi
na maabara za kisasa katika kata za kimkakati na makao makuu ya tarafa hizo. - Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali imepeleka shilingi bilioni 37.5 zilizotokana
na makusanyo ya tozo ya miamala ya simu kwenye Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa vituo
vya afya kwenye tarafa 150 kati ya tarafa 207. Kila kituo cha afya kimepelekewa shilingi
milioni 250 kwa ajili ya kuanza ujenzi huo. Natoa maelekezo kwa watendaji wote wa
Serikali za Mitaa kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kuakisi
thamani ya fedha kwenye utekelezaji wa miradi hiyo.
MAANDALIZI YA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA,
JANUARI 2022 - Mheshimiwa Spika, sote tunafahamu kwamba jana tarehe 9 Septemba, 2021
vijana wetu wa darasa la saba walimaliza mtihani wa Taifa wa Elimu ya Msingi ulioanza
tarehe 8 Septemba, 2021. Hivyo basi, nitumie fursa hii kuwapongeza na kuwaombea
Mwenyezi Mungu awajalie wote wafaulu vizuri na kujiunga na kidato cha kwanza, vyuo vya
ufundi na kujiendeleza na taaluma nyinginezo. - Mheshimiwa Spika, tangu kuanza kwa utekelezaji wa Sera ya Elimumsingi bila
Ada kumekuwa na mwitikio mzuri wa mahudhurio ya wanafunzi na hivyo kuongeza idadi ya
wahitimu katika mitihani ya kujipima na kumaliza elimu ya msingi. Ongezeko hilo la idadi ya
wahitimu, lilisababisha changamoto ya kutokuwepo kwa miundombinu ya elimu ya kutosha
hususan madarasa ya kuweza kupokea wahitimu wa darasa la saba waliofaulu kujiunga na
kidato cha kwanza.
4
- Mheshimiwa Spika, kufuatia hali hiyo, Serikali ilitoa maelekezo kwa watendaji wa
Serikali za Mitaa kuhakikisha wanatumia takwimu zilizopo kupanga maoteo na kutenga
fedha katika mipango na bajeti ya kila mwaka ili miundombinu ya elimu, samani na shule
hitajika viwepo kwa wakati. - Mheshimiwa Spika, maelekezo hayo, yalilenga kuiwezesha Serikali kutambua
mahitaji ya miundombinu ya elimu yatakayokidhi idadi hiyo ya wanafunzi na hivyo
kuhakikisha miundombinu hiyo inaandaliwa mapema. Katika mwaka 2021, makadirio
yanaonesha kuwa wanafunzi 934,706 sawa na asilimia 83.68 ya wanafunzi 1,115,041
waliohitimu mtihani wa darasa la saba wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza ifikapo
Januari, 2022. - Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika
shule za sekondari, Serikali imetumia shilingi bilioni 33.73 kwa ajili ya kujenga maboma
2,699 kati ya maboma 4,539 ya vyumba vya madarasa kwenye maeneo mbalimbali nchini.
Fedha hizo zinatokana na tozo ya miamala ya simu. - Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba tayari
Serikali imepeleka shilingi bilioni saba kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma 560 ikiwa ni
awamu ya kwanza. Aidha, maboma 1,840 yatakayogharimu shilingi bilioni 23
yatakamilishwa kupitia ruzuku ya Serikali Kuu. - Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kurejea maelekezo niliyoyatoa wakati
nikifungua mafunzo elekezi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa kwamba
wahakikishe miundombinu hiyo inakamilika kwa wakati. Lengo la Serikali ni kuona vijana
wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwakani wanapokelewa na kuanza masomo
yao kwa wakati.
BEI ELEKEZI YA MAFUTA - Mheshimiwa Spika, tarehe 31 Agosti, 2021 Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati nchini
(EWURA) ilitangaza bei mpya elekezi kwa bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba ambapo
ilionesha kupanda kwa bei za bidhaa hizo. Kufuatia taarifa hiyo, na malalamiko ya wananchi
juu ya kupanda kwa bei za bidhaa hizo, tarehe 1 Septemba 2021, Serikali ilisitisha bei mpya
zilizotangazwa na EWURA ili kufanya mapitio ya kina ya kupanda huko kwa bei. - Mheshimiwa Spika, tulichukua hatua hizo kutokana na ukweli kwamba kupanda
kwa bei ya mafuta huwaumiza wananchi hususan wale wa hali ya chini. Kwa kulitambua
hilo, tarehe 2 Septemba, 2021, niliunda timu maalumu ya uchunguzi. - Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mengine timu hiyo inafuatilia kupanda kwa
bei za bidhaa za mafuta mara kwa mara hususani petroli, dizeli, mafuta ya taa na ndege na
kisha kuishauri Serikali hatua stahiki za kuchukuliwa. Aidha, nimeielekeza timu hiyo
ijiridhishe kuhusu utitiri wa tozo kwenye bidhaa za mafuta na kuja na mapendekezo ya
namna nzuri ya kushughulikia suala hilo. - Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kuwa timu hiyo tayari
imeanza kutekeleza majukumu yake tangu tarehe 2 Septemba, 2021. Hali kadhalika,
itakapokamilisha taarifa yake Serikali itatoa mwelekeo wa yale yatakayopendekezwa.
MFUMO WA STAKABADHI ZA MAZAO GHALANI NA USHIRIKA
- Mheshimiwa Spika, miongoni mwa maeneo ambayo Serikali inayapa msukumo wa
kutosha ni masoko na mifumo ya mauzo ya mazao ya wakulima. Serikali inachukua hatua
hizi ili kuhakikisha kuwa wakulima wanapata tija na kunufaika na mazao yao. Katika
kutimiza azma hiyo, Serikali imeondoa mifumo isiyo rasmi ya ununuzi wa mazao ambayo
imekuwa ikiwakandamiza wakulima na kuwanufaisha baadhi ya wanunuzi wasiokuwa
waaminifu. Mathalan, tuliondoa mifumo kama vile kangomba, butula, chomachoma,
kula maua, njemke na mingineyo ambayo ilikuwa ikimpunja na kumnyonya mkulima. - Mheshimiwa Spika, kwa mantiki hiyo, Serikali imekuwa ikisimamia kikamilifu
mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani ambao umeonesha mafanikio makubwa katika
uuzaji wa mazao yakiwemo korosho, ufuta, dengu, choroko na kakao. Kwa lugha nyingine,
ufanisi wa mfumo huo, umekuwa kichocheo katika kupunguza umaskini na kuongeza
uchumi wa nchi na wakulima kwa ujumla. - Mheshimiwa Spika, taarifa zinaonesha kuwa kuuza mazao kupitia mfumo wa
stakabadhi ghalani na ushirika kunatoa nguvu ya pamoja kwa wakulima katika upatikanaji
wa masoko sambamba na kuimarisha bei ya mazao husika. Minada iliyofanyika imesaidia
kuongezeka kwa bei ya mazao yaliyotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ikiwemo
korosho, ufuta, dengu, choroko na kakao. - Mheshimiwa Spika, mwaka 2020 bei ya choroko iliongezeka kutoka shilingi 600
kwa kiwango cha chini hadi 800 kiwango cha juu kwa kilo na kufikia shilingi 900 hadi
1,300 kwa kilo katika vituo vya Magu, Uzogele, Igunga na Manyoni. Kadhalika, hivi
karibuni tumeona bei ya kakao ikiongezeka maradufu kutoka shilingi 2,500 hadi 5,000
kwa kilo baada ya kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani. - Mheshimiwa Spika, kwa msingi huo, natoa maelekezo kwa Wizara ya Kilimo
kushirikiana kwa karibu na vyama vya ushirika na vyama vya msingi katika kuhakikisha
wanawawezesha wakulima kupata elimu na manufaa ya kutumia mfumo wa stakabadhi
ghalani bila usumbufu ili uwapatie tija. - Mheshimiwa Spika, ni kweli mfumo wa stakabadhi ghalani unahitaji miundombinu
ya maghala. Hata hivyo, changamoto hizo zinaendelea kufanyiwa kazi ili mazao mengi zaidi
yaingizwe kwenye mfumo huo mwaka hata mwaka na kuleta tija zaidi kwa wakulima. - Mheshimiwa Spika, rai yangu kwa wakulima na wanunuzi wa mazao ni kwamba,
mfumo wa stakabadhi ghalani ndiyo pekee uliothibitika na kuonesha matokeo makubwa
yenye manufaa. Hivyo basi, tuendelee kuuimarisha katika mazao yote ya biashara nchini ili
kuleta mafanikio kwa wakulima na Taifa kwa ujumla.
UNUNUZI WA NAFAKA NCHINI - Mheshimiwa Spika, Serikali imefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuhamasisha
uzalishaji wa mazao ya chakula hususan nafaka pamoja na mazao ya biashara. Ongezeko
hili la uzalishaji linakwenda sambamba na jitihada za Serikali za kuimarisha masoko ya
ndani ya mazao pamoja na kutafuta masoko ya nje. - Mheshimiwa Spika, pamoja na kuboresha mifumo ya masoko, Serikali
inahamasisha ujenzi wa viwanda vya uchakataji wa mazao yanayozalishwa hapa nchini ili
kuimarisha bei ya mazao hayo na hivyo kumpatia tija mkulima.
- Mheshimiwa Spika, baada ya kuanza kwa msimu wa ununuzi wa mahindi hususan
katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, tulipokea malalamiko ya wananchi kuhusu umbali wa
vituo vya kununulia mahindi na bei kutoridhisha. Kama mnavyofahamu, kwa kiasi kikubwa
ununuzi wa mahindi nchini hufanywa na wafanyabiashara binafsi. Hata hivyo, ili kuimarisha
bei ya mahindi, Serikali hutoa fedha kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na
Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB). - Mheshimiwa Spika, jana tarehe 9 Septemba 2021, Bunge lako tukufu lilipokea
hoja binafsi kutoka kwa Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo na kuungwa
mkono na Waheshimiwa Wabunge. Hoja hiyo, ililenga kuishauri Serikali kuingilia kati soko la
mahindi ili kunusuru wakulima wa zao hilo. - Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa shilingi bilioni 15 kwa ajili kuwezesha Wakala
wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kununua mahindi maeneo mbalimbali nchini. Pia,
Serikali ilitoa kwa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko shilingi bilioni 10 kuongeza
mtaji wa ununuzi wa mazao. - Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa kiasi hicho cha fedha ni kidogo
ukilinganisha na uzalishaji wa mahindi uliopo. Hivyo, Serikali imesikia kilio cha wakulima
kupitia Waheshimiwa Wabunge na kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa wakulima
wa mahindi wanapata soko la mahindi waliyozalisha. - Mheshimiwa Spika, tayari Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, ametoa shilingi bilioni 50 na ununuzi utaanza Jumatatu, tarehe
13 Septemba, 2021. Hivyo, Wizara iendelee kutafuta masoko ya mahindi kwa
kukamilisha mikataba mipya ya ununuzi wa mahindi na nchi za Sudan ya Kusini, DRC na
Zimbabwe. - Mheshimiwa Spika, Serikali pia imeruhusu wafanyabiashara kutafuta masoko ya
nje ya nchi ambapo vibali vya usafirishaji hutolewa kupitia Ofisi za Wakuu wa Wilaya. Aidha,
uuzaji wa chakula utafanywa kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na
hifadhi ya kutosha ya chakula. Niendelee kusisitiza Wizara kushirikiana na Sekta Binafsi
katika kuongeza thamani ya mazao yetu ikiwemo mazao ya nafaka badala ya kuyauza nje
yakiwa hayajaongezwa thamani. - Mheshimiwa Spika, naiagiza Wizara ya Kilimo kuisimamia kwa karibu NFRA na CPB
ili zinunue mahindi ya wakulima pekee, tena watoke ndani ya nchi. Aidha, ongezeni vituo
vya kununulia mahindi hadi wilayani na kwenye miji midogo. - Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine, Serikali inafuatilia mwenendo wa
upatikanaji wa mbolea ili kuhakikisha bidhaa hiyo inapatikana kwa wingi na bei nafuu.
Lengo la Serikali ni kuwezesha wakulima kumudu gharama za mbolea.
UJENZI WA MJI WA SERIKALI - Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa Mji wa Serikali, mradi ambao
unatekelezwa kwa ufanisi mkubwa. Itakumbukwa kuwa katika awamu ya kwanza, Wizara
23 zilijenga ofisi zake na kuhamishia watumishi wapatao 18,300 jijini Dodoma. Aidha,
ujenzi wa majengo ya kudumu ya wizara 23 na taasisi zake utaanza tarehe 30 Septemba, - Ujenzi huo, utahusisha ipasavyo kampuni za ujenzi za umma na binafsi.
- Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kumshukuru na kumpongeza Mheshimiwa
Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia shilingi
bilioni 300 zitumike katika awamu ya pili ya ujenzi huo. Kadhalika, shilingi bilioni 300
nyingine zitatolewa kadri ujenzi unavyoendelea. Hivi sasa, ujenzi wa miundombinu wezeshi
ikiwemo barabara, majisafi na majitaka, umeme, gesi, mifumo ya TEHAMA, huduma za
zimamoto na upandaji miti unaendelea vizuri na kasi kubwa.
TAHADHARI DHIDI YA UVIKO-19 - Mheshimiwa Spika, Tanzania na dunia kwa ujumla bado imeendelea kupambana
na ugonjwa wa virusi vya korona maarufu kama UVIKO-19. Janga limesababisha baadhi ya
ndugu zetu kupoteza maisha na wengine kuendelea kuugua. Hivyo basi, hatuna budi
kuendelea kuchukua tahadhari kwa kujikinga na maambukizi ya UVIKO-19. - Mheshimiwa Spika, ninawasihi Waheshimiwa Wabunge wenzangu na wananchi
wote, tufuate maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na pale mtu anapoona dalili
ambazo hazielewi, awahi kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kilicho karibu ili
afanyiwe uchunguzi na kupatiwa matibabu. - Mheshimiwa Spika, katika hatua nyingine ya kukabiliana na UVIKO-19, tarehe 28
Julai, 2021 Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
alizindua rasmi kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo. Hivi sasa, chanjo hiyo inapatikana
maeneo yote nchini katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma ya afya wilayani na
mikoani. - Mheshimiwa Spika, niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge wenzangu na wananchi
wote kuwa chanjo hii ni salama na haina madhara yoyote. Chanjo hiyo ambayo
imethibitishwa na watalaamu na maabara zetu, ni hiyari lakini ni muhimu. Hivyo, niwaombe
twendeni tukachanje ili kukabiliana na janga hili.
MATUMIZI YA MITANDAO - Mheshimiwa Spika, hivi karibuni kumejitokea tabia ya baadhi ya watu kutumia
vibaya haki ya uhuru wa mawazo na mifumo mbalimbali ya mawasiliano. Matumizi mabaya
ya mitandao yamesababisha kusambazwa kwa taarifa za upotoshaji, kashfa, kutisha, na
wakati mwingine kudhalilisha watu, kikundi au viongozi. - Mheshimiwa Spika, katika kulinda na kutunza usalama, amani, maadili, umoja na
mshikamano wa nchi ninawaagiza Mawaziri wa Mambo ya Ndani na mwenzake wa Habari
na Teknolojia ya Mawasiliano watumie sheria, kanuni na taratibu zilizopo kuhakikisha
vitendo na mienendo hiyo inadhibitiwa nchini.
MICHEZO - Mheshimiwa Spika, nyote mtakubaliana nami kwamba kumekuwepo na mwamko
mkubwa wa masuala ya sanaa, burudani na michezo nchini. Hivi sasa, michezo imekuwa
chanzo kikubwa cha biashara, utalii, kuimarisha afya na ajira kwa vijana wetu. Kwa
kuzingatia hilo, Serikali imeendelea kuchukua hatua za makusudi za kukuza michezo nchini.
Hatua hizo zinahusisha kuundwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Michezo na kurejesha
mashindano ya UMITASHUMTA, UMISSETA na SHIMIWI.
- Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu
Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia kuanzishwa kwa Mfuko
wa Maendeleo ya Michezo nchini na kukubali kudhamini mashindano ya wanawake ya
CECAFA ili kutoa motisha kwa wanawake kushiriki zaidi katika michezo. Mashindano hayo,
yatajulikana kama Samia Cup sambamba na Kagame Cup kwa upande wa wanaume. - Mheshimiwa Spika, Mfuko huo, utasaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya
kuziandaa vyema timu zetu za Taifa za michezo mbalimbali na kuziwezesha kushiriki kwa
tija katika mashindano na michezo ya kimataifa. Pia, utatumika kuimarisha miundombinu ya
michezo na upatikanaji wa vifaa vya michezo, kuendeleza na kuwezesha shule na vituo vya
umahiri wa michezo, kuendesha programu za mafunzo ili kupata wataalaamu wa kutosha,
kuwezesha programu za michezo kwa jamii na mashindano ya kitaifa na kimataifa. - Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kueleza, michezo ni biashara na imekuwa
chanzo muhimu cha ajira hususan kwa vijana. Aidha, ibara ya 243 ya Ilani ya Uchaguzi ya
Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 inaielekeza Serikali kuanzisha mfumo thabiti wa
michezo ya kulipwa ili kulinda na kuendeleza vipaji vilivyopo kwa manufaa ya Taifa letu na
vijana kujipatia ajira kwa kutumia vipaji vyao. Tayari, Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa
(BMT) imefanyiwa mabadiliko na kuruhusu michezo ya kulipwa na baadhi ya timu zetu
zimeshaingia kwenye mfumo huo. - Mheshimiwa Spika, kutokana na utekelezaji wa sheria hiyo, hivi karibuni,
tumeshuhudia watalaamu wa michezo na wachezaji kutoka katika mataifa makubwa
yaliyoendelea kimichezo wakija nchini kutafuta ajira kupitia michezo. Vilevile, tumeshuhudia
uwekezaji mkubwa kwenye vilabu vyetu vikubwa nchini hususan Azam, Simba na Yanga na
kuvifanya viendeshwe kibiashara. - Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kwanza kuupongeza uongozi wa Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) chini ya Rais Wallace Karia kwa usimamizi mzuri wa soka nchini. Pili,
nawapongeza sana wawekezaji na watendaji wa vilabu vya Azam, Simba na Yanga kwa
uwekezaji mkubwa na usimamizi mzuri wa vilabu hivyo kwenye soka letu ambao umeanza
kuzaa matunda. - Mheshimiwa Spika, ninataka niwahakikishie wadau na wapenzi wa michezo kuwa
Serikali itaendelea kuimarisha na kuvutia uwekezaji mkubwa katika tasnia ya michezo.
Lengo ni kuibua na kuendeleza vipaji vya vijana wetu kimichezo ili waweze kushindana
katika masoko ya michezo ya ndani na nje ya nchi, na hivyo kuimarisha ajira, mapato
yatokanayo na shughuli za michezo pamoja na mchango wa sekta ya michezo katika pato la
Taifa. - Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuipongeza timu yetu ya Taifa ya Mpira wa
Miguu (Taifa Stars) kufuatia ushindi wa mabao matatu kwa mawili dhidi ya Madagascar na
hivyo kuongoza KUNDI J katika hatua ya pili ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia mwakani
nchini Qatar. Vilevile, tunaitakia kila la heri timu yetu ya wanawake ya kriketi inayoshiriki
mashindano ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia la mchezo huo nchini Botswana na timu
yetu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) itakayoshiriki mashindano ya COSAFA nchini
Afrika Kusini kuanzia tarehe 28 Septemba, 2021 pamoja na kuitakia mafanikio timu yetu ya
mchezo wa wavu inayoendelea kushiriki mashindano ya Afrika ya mchezo huo nchini
Rwanda. Ninavitakia kila la heri pia vilabu vyetu vya Azam, Biashara United, Simba na
Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii pia kukipongeza kituo cha matangazo cha
Azam (Azam Media) hususan upande wa matangazo ya runinga kwa kuuibua na
kuutangaza vyema mchezo wa masumbwi nchini. Juhudi hizo za Azam Media
wakishirikiana na wadau wengine zimewezesha wanamasumbwi wetu kutumia vizuri fursa
hiyo kukuza vipaji vyao.
Mheshimiwa Spika, niwapongeze mabondia wetu Twaha Kiduku kwa kumtwanga
Dulla Mbabe katika pambano lililovuta hisia za Watanzania wengi. Vilevile, nimpongeze
bondia Hassan Mwakinyo kwa kumdunda mpinzani wake Mnamibia Julius Indongo kwa TKO
na kutetea mkanda wake wa Chama cha Ngumi Afrika (ABU). Wanamasumbwi wetu
wameendelea kuifanya Tanzania itambulike zaidi ulimwenguni. Sasa tunasubiri pambano la
watani Mwakinyo dhidi ya Kiduku.
HITIMISHO
Mheshimiwa Spika, nihitimishe hotuba yangu kwa kumshukuru Katibu wa Bunge
na watendaji wa ofisi ya Bunge kwa kazi kubwa ya kuratibu vikao vya mkutano huu. Aidha,
niwashukuru watendaji wa Serikali kwa kufanikisha shughuli zilizopangwa na Bunge lako
tukufu kwa weledi na ufanisi mkubwa.
Mheshimiwa Spika, kipekee, niwashukuru wanahabari kwa kufikisha habari
kuhusu mkutano huu kwa wananchi. Nivishukuru pia vyombo vya ulinzi na usalama kwa
huduma wanazozitoa kwa washiriki wa Bunge hili bila kuwasahau madereva
waliotuhudumia wakati wote tukiwa hapa Bungeni.
Mheshimiwa Spika, natambua kuwa baada ya mkutano huu Waheshimiwa
Wabunge wenzangu watakuwa wakirejea majimboni kwao kuendelea na shughuli za
kuwahudumia wananchi ikiwa ni pamoja na kuwaeleza mambo yaliyojiri hapa Bungeni. Kwa
hiyo, niwatakie safari njema na niwaombe kuwa mkawaeleze wananchi pia kuhusu
matarajio yetu kwao na kuwasihi waendelee kutuunga mkono kusukuma mbele gurudumu
la maendeleo.
Mheshimiwa Spika, tarehe 19 Oktoba 2021, ikitegemewa na mwandamo wa
mwezi, ndugu zetu Waislamu wataadhimisha Mazazi ya Mtume Muhammad Swalla Allahu
Alayh Wasallam. Hivyo, nitumie nafasi hii kuwatakia kila la heri katika maandalizi na
hatimaye maadhimisho ya shughuli hiyo ya maulid ya kuadhimisha Mazazi ya Mtume
Muhammad Swalla Allahu Alayh Wasallam.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, sasa, naomba kutoa hoja kwamba
Bunge lako tukufu liahirishwe hadi tarehe 2 Novemba, 2021 siku ya Jumanne, saa tatu
kamili asubuhi litakapokutana tena katika ukumbi huu jijini Dodoma.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
Yanga katika uwakilishi wao kwenye michuano ya Shirikisho na Ligi ya Mabingwa ya Chama
cha Soka barani Afrika (CAF).
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *