RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. HusseinAli Mwinyi amesema ili Taifa liweze kufanikisha matarajio ya kukuzaUchumi katika mwaka wa Pili wa Uongozi wa Serikali ya Awamu yanane, halina budi kuendelea kudumisha amani, uwajibikaji pamoja nawatendaji kujenga uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.Dk. Mwinyi ametoa indhari hiyo katika Hotuba aliyotoa kwa wananchi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi amesema ili Taifa liweze kufanikisha matarajio ya kukuza
Uchumi katika mwaka wa Pili wa Uongozi wa Serikali ya Awamu ya
nane, halina budi kuendelea kudumisha amani, uwajibikaji pamoja na
watendaji kujenga uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Dk. Mwinyi ametoa indhari hiyo katika Hotuba aliyotoa kwa wananchi katika
kilele cha maadhimisho ya kutimiza mwaka mmoja wa Uongozi wake, hafla
iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip iliopo Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
Amesema katika mwaka wa Pili wa Uongozi wa Awamu ya Nane, Serikali
imekopa jumla ya Shilingi Bilioni 460 kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF)
ambazo shiligni Bilioni 230 kati ya fedha hizo zitatumika kufanikisha miradi
katika sekta mbali mbali za kijamii, ikiwemo Afya, elimu, maji safi na
salama na umeme pamoja na kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Alisema Shilingi Bilioni 230 zilizobaki zitatumika kwa ajili ya kulipia madeni
ya Wazabuni, kulipa fidia mbali mbali pamoja na kulipia haki mbali mbali za
wafanyakazi.
Alisema fedha hizo (bilioni 230) zitakazoingizwa katika shughuli za
kiuchumi ni nyingi sana na ni wazi kuwa zitaleta faida kubwa kwa Taifa
pamoja na kurahisha maisha kutokana na mzunguko wa fedha.
Hivyo, alisema matarajio hayo yatakamilika tu endapo wananchi
wataendelea kudumisha amani iliopo, sambamba na watendaji kuanzia
ngazi za chini za uongozi kuwajibika ipasavyo na kufanya kazi zao kwa
uadilifu, hususan katika suala la tenda.
Alieleza kuwa katika kipindi kilichopita miradi mingi ilishindwa kukamilishwa
vyema kwa sababu ya Rushwa na kubainisha viashiria vilivyoanza
kujichomoza na kusisitiza kwamba yeyote atakaejaribu kuchota fedha hizo
hatomuachia.
Rais Dk.Mwinyi alitoa indhari juu ya matumizi stahiki ya fedha hizo, huku
akiahidi kuwachukulia hatua kali za kisheria watendaji wote
watakaojihusisha na udokozi au upotevu wa fedha hizo.
Katika hatua nyengine, Dk. Mwinyi alimshukuru Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa
alizochukua kufanikisha kupatikana kwa mkopo huo pamoja na ukaribu
wake kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao umekuwa chachu ya
kuondokana na changamoto mbali mbali zinazojitokeza.
Aidha, Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imefanya uamuzi wa kuwalipa fedha zao (kiasi cha Shilingi Bilioni 38.7)
wahanga wote wa iliokuwa Masterlife, ikiwa ni hatua ya kuwaondolea
usumbufu wa maisha wananchi masikini walioweka fedha hizo.
Kitengo cha habari,
Ikulu Zanzibar
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *