JAJI MKUU ASEMA KUNA HAJA KUBORESHWA KWA MIFUMO YA TEHAMA YA MAHAKAMA

JAJI MKUU ASEMA KUNA HAJA KUBORESHWA KWA MIFUMO YA TEHAMA YA MAHAKAMA

JAJI Mkuu wa Tanzania,Profesa Ibrahimu Juma amesema kuna haja ya kuboreshwa  kwa mifumo ya TEHAMA ya Mahakama katika kusaidia wananchi   katika utoaji huduma na kukuza uchumi hali hiyo inatokana na mifumo mingi ya Mahakama kuwa na changamoto yakutosomana  na hivyo kutoleta manufaa kwa wananchi. Profesa Juma ametoa maelezo hayo  leo   Januari 27,2022  Jijini Dodoma mara

JAJI Mkuu wa Tanzania,Profesa Ibrahimu Juma amesema kuna haja ya kuboreshwa  kwa mifumo ya TEHAMA ya Mahakama katika kusaidia wananchi   katika utoaji huduma na kukuza uchumi hali hiyo inatokana na mifumo mingi ya Mahakama kuwa na changamoto yakutosomana  na hivyo kutoleta manufaa kwa wananchi.

Profesa Juma ametoa maelezo hayo  leo   Januari 27,2022  Jijini Dodoma mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali yanayoshiriki maonesho ya wiki ya Sheria ambayo Kitaifa yanafa katika Viwanja vya Nyerere Skwea Jijini Dodoma.

Hata hivyo Jaji Mkuu amezungumzia kuhusu Sheria ya adhabu ya kunyongwa.

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo akiwemo Afisa Uchunguzi wa TAKUKURU Grabriella  Gabriel,Mwanasheria wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA,Lilian Mollel na Kaimu Katibu wa Tume ya marekebisho ya Sheria Nchini,Zainabu Chanzi wakaeleza huduma wanazozitoa katika wiki ya Sheria.

Maadhimisho ya Wiki ya Sheria kwa mwaka 2022 yanakwenda sambamba na kaulimbiu isemayo”Dhama za Mapinduzi ya nne ya viwanda, na kilele  ni Februari Mosi Mwaka huu na mgeni rasmi anatarajiwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »