SERIKALI YAANZA HATUA ZA UTOAJI ELIMU YA UFUGAJI MASHULENI

SERIKALI YAANZA HATUA ZA UTOAJI ELIMU YA UFUGAJI MASHULENI

Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Abdallah Ulega amesema serikali imeanza hatua za utoaji elimu ya ufugaji kwa wanafunzi kwa kuanzisha Club zitakazowajengea uwezo wa ufugaji na kuwapatia ajira hata baada ya kumaliza masomo yao. Amesema hayo katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya kukusanyia na kusindika bidhaa za maziwa kwa vyama

Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Abdallah Ulega amesema serikali imeanza hatua za utoaji elimu ya ufugaji kwa wanafunzi kwa kuanzisha Club zitakazowajengea uwezo wa ufugaji na kuwapatia ajira hata baada ya kumaliza masomo yao.

Amesema hayo katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya kukusanyia na kusindika bidhaa za maziwa kwa vyama vya ushirika wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Alisema Club hizo za kutoa elimu ya ufugaji wa aina mbalimbali za mifugo zitaanzishwa hasa kwenye shule zenye maeneo makubwa ili wanafunzi wapate eneo la kutosha kwa ufugaji

Mheshimiwa Ulega alisema madarasa hayo kwa wanafunzi shuleni yataanzishwa katika mikoa ambayo wananchi wake hawana kabisa ujuzi wa ufugaji sambamba na ujuzi wa usindikaji wa maziwa.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »