Mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labor Part (TLP), Augustino Mrema leo Alhamisi Machi 24, 2022 ameamua kuacha ukapela na kufunga ndoa na Doreen Kimbi. Ndoa hiyo imefungwa katika kanisa Katoliki Parokia ya Uwomboni Kiraracha mkoani Kilimanjaro. Mke wa mzee Mrema anayejulikana kwa jina la Doreen Kimbi amesema kuwa atamrudisha mzee Mrema ujanani. “Mpaka kufikia hivi
Mwenyekiti wa chama cha Tanzania Labor Part (TLP), Augustino Mrema leo Alhamisi Machi 24, 2022 ameamua kuacha ukapela na kufunga ndoa na Doreen Kimbi.
Ndoa hiyo imefungwa katika kanisa Katoliki Parokia ya Uwomboni Kiraracha mkoani Kilimanjaro.
Mke wa mzee Mrema anayejulikana kwa jina la Doreen Kimbi amesema kuwa atamrudisha mzee Mrema ujanani.
“Mpaka kufikia hivi alivyo nimemfanya hivi. Katika kipindi cha uchumba nimemweka kuwa sawa, vitu vyote anavyohitaji anavipata. Kwa sasa amebadilika, nimeamua mwenyewe na sijashurutishwa na mtu na watarajie kuona anapendeza, nataka hadi awe kijana” amesema Doreen.
Mrema anaoa baada ya Mke wake wa kwanza Rose Mrema kufariki September, 2021.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *