Na Mwandishi Wetu-DodomaJuni 17 2022 Mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amewataka wakuu wa shule mkoani hapa kuendelea kuwapokea wanafunzi wa shule bila ya kujali Ada wala michango ya shule mpaka hapo waraka wa kutolipa Ada utakapotolewa. Agizo hilo amelitoa leo jijini Dodoma wakati wa kikao cha wakuu wa shule kilichofanyika kwenye ukumbi wa
Na Mwandishi Wetu-DodomaJuni 17 2022
Mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amewataka wakuu wa shule mkoani hapa kuendelea kuwapokea wanafunzi wa shule bila ya kujali Ada wala michango ya shule mpaka hapo waraka wa kutolipa Ada utakapotolewa.
Agizo hilo amelitoa leo jijini Dodoma wakati wa kikao cha wakuu wa shule kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa dodoma.
Aidha Mtaka amewataka wakuu wa shule wasiwalazimishe watoto kununua vitu kwenye maduka ya shule.
Mtaka Amesema michango yote ya shule hisitofautiane na shule zingine na michango hisizidii 150000/= Ili kumsaidia Mtoto wa hali ya chini aweze kumudu michango huo. Pamoja na hayo ameomba wakuu hao wasikwanzike Kwa mabadiliko haya ila washirikiane na kuwasaidia watoto wasiojiweza Ili watoto hao wapate elimu.
KWa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Msakwalo Halberto Virus Kaliwabu Ameiomba Serikali kuongeza walimu kwani hapo mawazo waliajiri walimu wakujitolea hivyo kutokana na Ada kutolewa kunachangamoto ya walimu kuendelea kujitolea.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *