SOKO KUU LA MCHINGA JIJINI DODOMA KUFUNGULIWA RASMI JULAI MOSI

SOKO KUU LA MCHINGA JIJINI DODOMA KUFUNGULIWA RASMI JULAI MOSI

Na Barnabas Kisengi-Dodoma Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma JOSEPH MAFURU  amesema ujenzi wa soko la wamachinga wa Jiji la Dodoma  umefika  asilimia 95 kukamilika na wanategemea ifikapo Julai mosi mwaka huu wafanya biashara hao wahamie na kuanza kufanya biashara zao katika soko hilo. Mategemeo tarehe 1 mwezi 7 mwaka huu ambapo hadi Sasa  wafanyabiashara 3000

Na Barnabas Kisengi-Dodoma


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma JOSEPH MAFURU  amesema ujenzi wa soko la wamachinga wa Jiji la Dodoma  umefika  asilimia 95 kukamilika na wanategemea ifikapo Julai mosi mwaka huu wafanya biashara hao wahamie na kuanza kufanya biashara zao katika soko hilo.

Mategemeo tarehe 1 mwezi 7 mwaka huu ambapo hadi Sasa  wafanyabiashara 3000 tayari  wamejisajiri Kwa  mfumo wa kielektroniki kufanya biashara kwenye soko hilo.
MAFURU amesema hayo wakati alipotembelewa na Wajumbe wa  Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania ( ALAT )   wakitembelea soko  la wamachinga jijini Dodoma.


Pia MAFURU amemshukuru  RAIS SAMIA SULUHU HASSAN Kwa kuongezae fedha kiasi Cha bilioni 2.5 ili kuweza kuhakikisha wanakamilisha mradi wa soko hilo.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tazania ALAT Mhe. Murshid Ngeze  amewaomba viongozi wa mkoa na viongozi wa Majiji kuendelea kutoa Elimu kwa wafanyabiashara wadogo Ili kuwaboreshea na kuwapatia elimu ili kuweza kuwafanya waweze kuafanya biashara zao katika maeneo mazuri na salama na yakiwa rafiki na wateja wao.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »