WALAJI WA POPO, PANYA WATAHADHARISHWA KUPATA HOMA YA MGUNDA

WALAJI WA POPO, PANYA WATAHADHARISHWA KUPATA HOMA YA MGUNDA

Na Barnabas Kisengi, Dodoma Serikali imetoa kauli juu ya  kuibuka kwa ugonjwa wa Homa ya mgunda uliotokea huko mkoani Lindi na kuenea kwa taarifa zinazodai kuwa nyama si salama kukiwa.Hayo yameelezwa  leo Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa huduma za mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga wakati akizungumza na waandishi wa Habari

Na Barnabas Kisengi, Dodoma


Serikali imetoa kauli juu ya  kuibuka kwa ugonjwa wa Homa ya mgunda uliotokea huko mkoani Lindi na kuenea kwa taarifa zinazodai kuwa nyama si salama kukiwa.
Hayo yameelezwa  leo Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa huduma za mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga wakati akizungumza na waandishi wa Habari kutolea ufafanuzi suala hilo ambapo amesema nyama inayouzwa kwenye mabucha yaliyosajiliwa ni salama na haina vimelea vya ugonjwa huo.


Aidha Prof. Nonga amewatahadharisha wananchi wenye tabia ya kula nyama za wanyama kama panya na popo kwani ni wanyama wenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na  kuepuka mwingiliano na wanyamapori.

Kwa upande wake msajili wa bodi ya nyama Tanzania Dkt. Daniel Mushi amesema Bodi hiyo inafanya kazi ya  ukaguzi kwenye mabucha yote hapa nchini ili kuhakikisha nyama inayouzwa inakuwa salama Kwa matumizi ya binadamu.

“Tumekuwa tukifanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maduka ya kuuzia nyama na kukagua ili kuhakikisha nyama inapo mfikia mlaji ikiwa salama kwa matumizi ya binadamu” amesema Dkt Mushi.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »