WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS SAMIA MAZISHI YA ABE

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS SAMIA MAZISHI YA ABE

Na Mwandishi Wetu Japan. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wa pili kushoto)  wakijiandaa kuweka maua wakati wa  mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Waziri Mkuu Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo  Abe yaliyofanyika  Tokyo nchini Japan Septemba 27, 2022. Wengine kutoka kushoto  ni mke wa Balozi wa Tanzania nchini Japan, Consolata Luvanda, Balozi wa Tanzania nchini Japan, Baraka Luvanda na

Na Mwandishi Wetu Japan.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wa pili kushoto)  wakijiandaa kuweka maua wakati wa  mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Waziri Mkuu Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo  Abe yaliyofanyika  Tokyo nchini Japan Septemba 27, 2022. Wengine kutoka kushoto  ni mke wa Balozi wa Tanzania nchini Japan, Consolata Luvanda, Balozi wa Tanzania nchini Japan, Baraka Luvanda na kulia ni Naibu Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wa pili kushoto)  wakiweka maua wakati wa mazishi ya kitaifa ya aliyekuwa Waziri Mkuu Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo  Abe yaliyofanyika  Tokyo nchini Japan Septemba 27, 2022. Kushoto ni mke wa Balozi wa Tanzania nchini Japan, Consolata Luvanda, na kulia ni Naibu Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.

Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

……………………………….

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameungana na wakuu wa nchi na viongozi mbalimbali 700 kutoka nchi 195 na mashirika ya kimataifa 23 kuweka mashada kwenye mazishi ya kitaifa ya Waziri Mkuu mstaafu wa Japan, Bw. Shinzo Abe.

Waziri Mkuu ambaye yuko Tokyo, Japan akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, ametoa heshima hizo za mwisho leo (Jumanne, Septemba 27, 2022) kwenye ukumbi wa Nippon Budokan akiwa ameambatana na mkewe Mary Majaliwa, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk, Balozi wa Tanzania nchini Japan, Balozi Baraka Luvanda na mkewe Consolata Luvanda.

Baada ya kutoa heshima za mwisho, Waziri Mkuu alikwenda kwenye Kasri la Kifalme la Akasaka, jijini Tokyo ambako hufanyika shughuli zote za Kiserikali ili kumfariji Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Fumio Kishida pamoja na mjane wa Bw. Shinzo Abe, Bibi Akie Abe. Alikuwa miongoni mwa viongozi wengine wa kitaifa 40 ambao walipata fursa hiyo.

Viongozi wengine wa kitaifa walioshiriki mazishi hayo ni Marais kutoka Vietnam, Sri Lanka, Makamu wa Rais kutoka Indonesia, Marekani, Ufilipino, Marais wastaafu wa Ufaransa, Ujerumani na Mfalme wa Falme za Kiarabu, mtawala wa Qatar na Amiri wa Kuwait. Mawaziri Wakuu 16 walihudhuria mazishi hayo.

Miongoni mwa mawaziri wakuu waliokuwepo ni Narendra Modi (India), Justin Trudeau (Canada), Han Duck-soo (Korea Kusini) na Antony Albanese (Australia). Wengine ni Mawaziri Wakuu wastaafu, Maspika, Majaji, wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mabalozi. Baadhi ya nchi na taasisi zilizowasilisha salamu za rambirambi, zilisomwa majina yao.  

Mapema asubuhi, wakazi wa Japan walijipanga kwenye misururu mirefu ili kupata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa kuweka mashada ya maua kwenye eneo maalum lililoandaliwa katika bustani nje ya ukumbi huo. Ukumbini kulikuwa na watu zaidi ya 4,300.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »