Na Barnabas Kisengi Dodoma Serikali kupitia wizara ya Elimu imeanza kuchukua hatua kufuatia ripoti iliyochapishwa kwenye vyombo vya habari juu ya uwepo wa baadhi ya shule zinayofundisha wanafunzi maadili mabaya, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma. Prof.Mkenda amesema kuwa Wizara ya
Na Barnabas Kisengi Dodoma
Serikali kupitia wizara ya Elimu imeanza kuchukua hatua kufuatia ripoti iliyochapishwa kwenye vyombo vya habari juu ya uwepo wa baadhi ya shule zinayofundisha wanafunzi maadili mabaya, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda Ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
Prof.Mkenda amesema kuwa Wizara ya Elimu sayansi na Teknolojia tayari Imeshamwaagiza Kamishina wa Elimu Tanzania, Mzibiti Ubora wa Shule Nchini na Mwanasheria wa Wizara ya Elimu wameanza uchunguzi katika hizo shule zilizotajwa na baada ya hapo watakuja na majibu.
“Hatuwezi kusema kesho au keshokutwa watupatie majibu maana ni suala linalohitaji uchunguza na kupatikane majibu ya usahihi ili tuepuke kuharakisha mambo alafu baadae mambo yakaharibika ndio maana tumemwagiza Kamishina aa elimu mwenyewe sio Mwakilishi na Mwanasheria wa Wizara na sio Mwakilishi tupate majibu yaliyokamilika,”Amesisitiza Prof.Mkenda
Waziri Mkenda amesema kuwa wizara imekusudia kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa namba maalumu kwaajili ya kutoa taarifa ya vitendo hivyo katika shule za umma au binafsi hapa Nchini
“Katibu Mkuu atatoa namba maalum kwa ajili ya kila mmoja kupiga simu pale ambapo atabaini kuna vitendo hivyo vichafu shuleni,”amesema Prof.Mkenda
Aidha Prof.Mkenda amesema kuwa Serikali itahakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa kwani vitaondoa uaminifu kwa wazazi juu ya kuwapeleka watoto wao shule.
Prof.Mkenda amesema kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itashirikiana na Wizara zingine za kisekta kupata ufumbuzi na kukomesha matukio kama hayo yanayotokea mashuleni.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *