Mamlaka ya mawasiliano Uganda yaamuru mitandao ya kijamii kufungwa.

Mamlaka ya mawasiliano Uganda yaamuru mitandao ya kijamii kufungwa.

Mamlaka ya mawasiliano ya Uganda imeyaamuru makampuni ya huduma za intaneti, kuifunga mitandao ya kijamii siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika. Katika barua ambayo shirika la habari la AFP limeipata, mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano ya Uganda UCC Bi. Irene Sewankambo ameyaagiza makampuni ya mawasiliano kusitisha mara moja matumizi ya mitandao ya kijamii na

Mamlaka ya mawasiliano ya Uganda imeyaamuru makampuni ya huduma za intaneti, kuifunga mitandao ya kijamii siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.

Katika barua ambayo shirika la habari la AFP limeipata, mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano ya Uganda UCC Bi. Irene Sewankambo ameyaagiza makampuni ya mawasiliano kusitisha mara moja matumizi ya mitandao ya kijamii na majukwaa ya kutuma ujumbe mtandaoni.

Uamuzi huo umetajwa wazi kuwa ni ulipaji kisasi wa hatua ya mtandao wa Facebook wa kufuta akaunti zinazounga mkono serikali zinazojaribu kudhibiti mjadala wa umma kuelekea uchaguzi mkuu.

Kampuni ya Facebook ilisema hapo jana kwamba akaunti hizo zinahusishwa na wizara ya habari na teknolojia.

Mitandao iliyowekwa katika orodha ya kufungiwa ni Facebook, Twitter, WhatsApp na Viber.

Baadhi ya mitandao tayari imeripotiwa kutopatikana kuanzia leo.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »