Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga, linamshikilia dereva Simon Pasian Tarimo miaka 37 mkazi wa Kimara jijini Dar es salaamkwatuhuma za kusafirisha mirungi bunda 1,685 sawa na kilogramu 133, akiwa ameweka kwenye jokofu linalotumika kuhifadhia jeneza lenye maiti wakati wa kusafirisha. Akitoa taarifa hiyo kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Blasius Chatanda amesema Simon Pasian
Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga, linamshikilia dereva Simon Pasian Tarimo miaka 37 mkazi wa Kimara jijini Dar es salaamkwatuhuma za kusafirisha mirungi bunda 1,685 sawa na kilogramu 133, akiwa ameweka kwenye jokofu linalotumika kuhifadhia jeneza lenye maiti wakati wa kusafirisha.
Akitoa taarifa hiyo kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Blasius Chatanda amesema Simon Pasian Tarimo alikamatwa majira ya saa 2:00 usiku katika Kijiji cha Manga, Kata ya Mkata, Tarafa ya Mazingara wilayani Handeni mkoani Tanga, ambapo mirungi hiyo ilikuwa ikisafirishwa kutoka Usangi kupelekwa Dar es Salaam, ikiwa imehifadhiwa kwenye gari maalumu la kubebea maiti.
Kamanda Chatanda amesem Simon Pasian Tarimo ameweka mifuko kwenye jokofu linalotumika kuhifadhi jeneza lenye maiti wakati wa kusafirisha kitendo ambacho ni kinyume cha matumizi ya gari hilo.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *