Matukio mbalimbali katika picha kwenye sherehe za CCM Kisonge-Zanzibar.

Matukio mbalimbali katika picha kwenye sherehe za CCM Kisonge-Zanzibar.

Picha na – OMPR – ZNZ.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Hemed Suleiman Abdulla Kulia akisalimiana na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM  Mkoa Mjini Mzee Borafia Silima Juma alipowasili Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 44 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar Bibi Cathelin Pita Nao akitoa maelezo wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya kutimia Miaka 44 ya Chama cha Mapinduzi hapo Kisonge Michenzani.
Msanii Issa Khamis kutokja Kikundi cha Tarab cha Culture akiimba Wimbo Maarufu wa Kuunganisha Vyama vha TANU na ASP Mnamo Mwaka 1977 wa Afro Mama Tunakuaga.
Malkia wa Mipasho Tanzania Qeen Khadija Omar Kopa akiimba wimbo Maarufu wa ukichunguza usichunguzew kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 44 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi. Hapo Mapinduzi Square.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla akikata Keki Maalum kuashiria kunoga kwa Sherehe za Miaka 44 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzui CCM Hapo Mapinduzi Square.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar  Dr. Abdulla Juma Sasadala {Mabodi} akitoa salamu wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya kutimia Miaka 44 ya Chama cha Mapinduzi hapo Kisonge Michenzani.
Msanii Munira wa Kikundi cha Taarab cha Big Star Chama  cha Mapindizo Mkoa akiimba wimbo mahsusi usemao CCM Chama cha kujivunia wakatimwa kuadhimisha Miaka ya 44 ya CCM Mapinduzi Square Michenzani.

Picha na – OMPR – ZNZ.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »