Dr. Gwajima amuagiza Katibu Mkuu Idara kuu ya maendeleo ya Jamii kuhakikisha anampatia taarifa kuhusu Fedha zinazotolewa na Serikali.

Dr. Gwajima amuagiza Katibu Mkuu Idara kuu ya maendeleo ya Jamii kuhakikisha anampatia taarifa kuhusu Fedha zinazotolewa na Serikali.

Na Barnabas kisengi Dodoma  February  24 2021 WAZIRI wa Afya,maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto,Dorothy  Gwajima amemuagiza Katibu Mkuu,Idara kuu ya maendeleo ya Jamii kuhakikisha anampatia   taarifa kuhusu Fedha zinazotolewa na Serikali kupitia halmashauri katika kuwawezesha wanawake kiuchumi. Hatua hiyo ya Waziri Gwajima imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kuwa hawajapata mikopo ambayo imekuwa ikitolewa na

Waziri wa Afya,maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto, Dkt. Dorothy  Gwajima

Na Barnabas kisengi Dodoma 

February  24 2021

WAZIRI wa Afya,maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto,Dorothy  Gwajima amemuagiza Katibu Mkuu,Idara kuu ya maendeleo ya Jamii kuhakikisha anampatia   taarifa kuhusu Fedha zinazotolewa na Serikali kupitia halmashauri katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Hatua hiyo ya Waziri Gwajima imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kuwa hawajapata mikopo ambayo imekuwa ikitolewa na Serikali katika kuwawezeshakiuchumi huku  wengine wakidai hawajui kama kuna Fedha hizo.

Kauli hiyo ameitoa leo Jijini Dodoma wakati akifungua kongamano la Chama cha Wataalam wa Maendeleo ya jamii DECOPATA lenye Lengo  la kuboresha utendaji kazi ambalo limewashirikisha  maafisa wa maendeleo ya jamii Nchini pamoja na wataalam wa maendeleo ya Jamii.

Hata hivyo amebainisha kuwa  dhamira ya Serikali ni kuiwezesha Tanzania ifikapo2025 iwe Nchi ya uchumi wa Kati ambapo jitihada za uwezeshaji wananchi kiuchumi hivi sasa Serikali imeshatoa jumla ya Shbil23.8zimetolewa na Serikali kwa wananchi katika kuwawezesha kiuchumi.

Sanjari na hilo amewataka Maafisa maendeleo ya Jamii kutimiza wajibu wao katika kuwasaidia wananchi  kuleta maendeleo kwakuanzisha vikundi,viwanda vya Kati ili waweze kujikwamua  kiuchumi huku akiwataka kuongeza kasi ya kutumia stadi katika kuielimisha Jamii hasa Kaya maskini ili kujitegemea kwa  kubadilisha fikra zao.

Amesema Serikali ya awamu ya tano  inatekeleza Miradi mbalimbali ya kisekta na kimkakati ikiwemo reli ya kisasa,Bomba la mafuta,mradi wa kufua umeme na katika kukamilisha miradi hiyo Serikali inahitaji ushiriki wa wananchi.

Katika hatua nyingine Waziri Gwajima ametoa tamko la kutaka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya kuambukiza kwakuzingata kanuni za afya ikiwemo kunawa mikono  huku akimwagiza Mfamasia wa Serikali kutoa maelekezo juu ya matumizi ya tiba za asili kwa wananchi.

Kwa upande wake Rais  wa Chama Cha Wataalam wa Maendeleo ya Jamii Nchini(CODEPATA),Wambura Sande amesema mipango ya Chama hicho ni pamoja na kuhamasisha wataalam kujiunga na chama kufanya maandalizi ,kuandaa mpango mkakati wa chama utakaotoa dira ya Chama ambapo pia wamempongeza Rais DK Magufuli kwa utendaji wake wa kazi ikiwemo kuhamishia makao makuu ya nchi Dodoma.

Kauli mbiu ya uchumi wa Kati Serikali imekuwa ikitekeleza mkakati wqkukuza viwanda vikubwa na vya Kati ili kuondokana na dhana ya kuagiza bidhaa toka nje.

Awali akimkaribisha Waziri katika kongamano hilo,Katibu Mkuu, Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii,Wizara ya Afya  Maendeleo ya Jamii jinsi wazee na watoto,John Jingu amesisitiza suala la maadili kwa maafisa maendeleo ya Jamii.

Kongamano hilo la siku mbili limewashirikisha Maafisa maendeleo ya jamii pamoja na wataalam wa maendeleo ya jamii takribani 200.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »