WAADVENTISTA WASABATO WAASWA KUACHA KUKATISHWA TAMAA NA VIKWAZO VYA ULIMWENGU.

WAADVENTISTA WASABATO WAASWA KUACHA KUKATISHWA TAMAA NA VIKWAZO VYA ULIMWENGU.

Mkurugenzi  idara ya Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kati Mwa TanzaniaK[CTF] Mchungaji David Mmbaga amewaasa Wakristo kuacha kukatishwa tamaa kutokana na vikwazo vya dunia kwani vikwazo vina makusudi maalum kwa maisha ya mwanadamu. Mchungaji Mmbaga amebainisha hayo leo Machi,6,2021  katika mahubiri ya ibaada kuu Kanisa la Waadventista Wasabato Mpwapwa mkoani Dodoma ambapo


Mkurugenzi  idara ya Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kati Mwa TanzaniaK[CTF] Mchungaji David Mmbaga amewaasa Wakristo kuacha kukatishwa tamaa kutokana na vikwazo vya dunia kwani vikwazo vina makusudi maalum kwa maisha ya mwanadamu.


Mchungaji Mmbaga amebainisha hayo leo Machi,6,2021  katika mahubiri ya ibaada kuu Kanisa la Waadventista Wasabato Mpwapwa mkoani Dodoma ambapo amebainisha kuwa vikwazo ni moja ya  hatua muhimu kwa maisha ya mwanadamu ili awe kuwa imara zaidi katika imani na maisha ya kawaida ya kila siku.

Sauti ya Mkurugenzi  idara ya Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kati Mwa TanzaniaK[CTF] Mchungaji David Mmbaga


Katika hatua nyingine, Mhubiri Mkuu katika Sabato ya  leo Machi 6,2021 Kanisa la Waadventista Wasabato Kizota jijini Dodoma Dkt.Herry Mhando ametoa hamasa kwa Washiriki kuwa Mstari wa mbele kwa kufanya kazi kwa bidii katika kujikwamua kiuchumi


Sauti ya Dkt.Herry Mhando


Aidha,Dkt.Mhando ametumia fursa hiyo kuhimiza washiriki kuwa na desturi ya kusoma Biblia mara kwa mara katika kuwajenga kiroho huku akitoa wito kuendelea kuchangia ili kufanikisha Mahubiri ya Kizota NET Event.

Sauti ya Dkt.Herry Mhando


Mahubiri ya Satelite ya Kizota Net Event yanatarajiwa kuanza Mwezi Juni,2021 na yatarushwa na vyombo  mbalimbali  vya Habari vikiwemo vya  Kanisa ambavyo ni Morning Star Radio,Hope Channel Tanzania na mnenaji Mkuu wa Mahubiri hayo ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Union Kuu ya Kusini Mwa Tanzania ,Mchungaji Mark Walwa Malekana.

Na Barnabas Kisengi

Dodoma March 6, 2021

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »