Uongozi wa klabu ya Yanga umefanya mazungumzo na aliyekuwa Kocha msaidizi wa kikosi hicho Juma Mwambusi ili kuja kukinoa kikosi cha Klabu hiyo. Hatua hiyo inakuja baada ya klabu hiyo kutangza kuvunja mkataba na aliyekuwa kocha Mkuu, Cedric Kaze mnamo March 07, 2021.Juma Mwambusi aliomba kuvunja mkataba wake na yanga hivi karibuni kwa madai ya
Uongozi wa klabu ya Yanga umefanya mazungumzo na aliyekuwa Kocha msaidizi wa kikosi hicho Juma Mwambusi ili kuja kukinoa kikosi cha Klabu hiyo. Hatua hiyo inakuja baada ya klabu hiyo kutangza kuvunja mkataba na aliyekuwa kocha Mkuu, Cedric Kaze mnamo March 07, 2021.
Juma Mwambusi aliomba kuvunja mkataba wake na yanga hivi karibuni kwa madai ya kuumwa lakini sasa yuko sawa kiafya na anaweza kurejea kukinoa kikosi hicho cha yanga
Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Dkt. Mshindo Msola amesema ” Mwambusi ataichukua timu kwa sasa wakati tunamtafuta Mwalimu mwingine, na kwa bahati nzuri Mwambusi aliondoka na kuaga vizuri, na klabu ilimsaidia kupata matibabau wakati anaumwa na tokea ligi inaanza tulikuwa naye hivyo sio kwamba ana ugeni na timu”
Dkt. Msindo Msola ameyasema hayo akiwa anamtangaza Juma Mwambusi kuwa Kocha wa Yanga kwa muda.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *