MAHITAJI YA DAMU SALAMA KATIKA JIJI LA DODOMA NI CHUPA HAMSINI KWA WIKI.

MAHITAJI YA DAMU SALAMA KATIKA JIJI LA DODOMA NI CHUPA HAMSINI KWA WIKI.

Mratibu wa Damu Salama jiji la Dodoma Jerome Malando amesema mahitaji ya Damu salama katika jiji la Dodoma ni chupa hamsini huku wito ukitolewa kwa  kila mmoja kuguswa kuchangia damu salama ili kuokoa maisha ya watu. Malando amebainisha hay oleo Machi,20,2020 katika kanisa la Waadventista Wasabato Kikuyu jijini  Dodoma wakati wa uchangiaji wa Damu Salama

Mratibu wa Damu Salama jiji la Dodoma Jerome Malando amesema mahitaji ya Damu salama katika jiji la Dodoma ni chupa hamsini huku wito ukitolewa kwa  kila mmoja kuguswa kuchangia damu salama ili kuokoa maisha ya watu.

Malando amebainisha hay oleo Machi,20,2020 katika kanisa la Waadventista Wasabato Kikuyu jijini  Dodoma wakati wa uchangiaji wa Damu Salama bure  katika kuadhimisha Juma la Matendo ya Huruma kanisa la Waadventista Ulimwenguni.

Mratibu huyo wa Damu salama katika jiji la Dodoma amesema damu ina mahitaji makubwa katika uhai wa binadamu na haiwezi kuzalishwa  katika kiwanda chochote hivyo ni muhimu kila mmoja kuguswa kuchangia damu ambapo jiji la Dodoma lina uhitaji wa chupa 50 za damu kila wiki.

Malando ametumia fursa hiyo kulipongeza kanisa la Waadventista Wasabato kwa kuwa na desturi ya kuadhimisha matendo ya huruma kwa kutoa misaada mbalimbali  kwa jamii ikiwemo kuchangia damu  huku Mzee wa kanisa la Waadventista Wasabato Kikuyu Elias Aron akielezea jinsi walivyoguswa katika utoaji wa damu salama .

Kwa upande  wao  baadhi ya washriki  kwa Kanisa la Waadventista Wasabato Kikuyu akiwemo Samwel Makumil,Deus Mchoo,Victoria Mkama pamoja na Paula Kazima wamesema suala la uchangiaji wa Damu ni sehemu ya ibaada katika kuokoa watu wenye matatizo mbalimbali.

Na Barnabas kisengi Dodoma.

 March 20 2021

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »