Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na wakuu wa taasisi mbalimbali za serikali. Baadhi ya mabadiliko Alphayo Kidata ameteuliwa kuwa kamishna wa mamlaka ya mapato Tanzania, nafasi aliyowahi kuitumikia kabla na uteuzi wake kutenguliwa na Rais Magufuli. Erick Hamis ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya usimamizi wa bandari
Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu na wakuu wa taasisi mbalimbali za serikali.
Baadhi ya mabadiliko
- Alphayo Kidata ameteuliwa kuwa kamishna wa mamlaka ya mapato Tanzania, nafasi aliyowahi kuitumikia kabla na uteuzi wake kutenguliwa na Rais Magufuli.
- Erick Hamis ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya usimamizi wa bandari baada ya aliyekuwa mkurugenzi wake, Deusdedith Kakoko kusimamishwa kazi kupisha uchunguzi
- Gerson msigwa ameteuliwa kuwa mkurugenzi wa idara ya habari kuchukua nafasi ya Dkt. Hassan Abbas ambae amebakia na nafasi yake ya katibu mkuu wizara ya habari. Kabla Msigwa alikuwa mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais, Ikulu
- Dkt. Jabir Kuwe ameteuliwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Eng. Kilaba.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *