RC KUNENGE AZIASA TAASISI NA MASHIRIKA YALIYOSAJILIWA KUTOA HUDUMA KWA JAMII KUFUATA MISINGI YA USAJILI.

RC KUNENGE AZIASA TAASISI NA MASHIRIKA YALIYOSAJILIWA KUTOA HUDUMA KWA JAMII KUFUATA MISINGI YA USAJILI.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge leo ameshiriki Mashindano ya Sita ya Kuhifadhi Quran takatifu ambapo ametoa wito kwa Mashirika yaliyopewa usajili kwa lengo la kusaidia jamii hususani yatima na wasiojiweza kuhakikisha wanatenda haki kwa walengwa. RC Kunenge amesema haipendezi kuona Shirika linapokea msaada wa vitu kwaajili ya kuasaidia Yatima, Makundi

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Aboubakar Kunenge leo ameshiriki Mashindano ya Sita ya Kuhifadhi Quran takatifu ambapo ametoa wito kwa Mashirika yaliyopewa usajili kwa lengo la kusaidia jamii hususani yatima na wasiojiweza kuhakikisha wanatenda haki kwa walengwa.

RC Kunenge amesema haipendezi kuona Shirika linapokea msaada wa vitu kwaajili ya kuasaidia Yatima, Makundi maalumu na waishio Katika Mazingira Magumu na kutumia msaada huo kujinufaisha wenyewe pasipo kuwafikia walengwa ambapo amesema kitendo hicho ni “ubabaishaji”.

Aidha RC Kunenge amesema ndani ya Jamii tumebarikiwa kuwa na Wadau wengi wanaopenda kusaidia watu wasiojiweza lakini uwepo wa Taasisi zisizofuata misingi ya usajili imekuwa ikiwavunja moyo Wadau.

Akizungumza kuhusu Mashindano hayo RC Kunenge amesema yanasaidia Jamii kuelewa kwa undani Vitabu vya dini Jambo linalojenga Jamii yenye maadili na hofu ya Mungu.

Hata hivyo RC Kunenge ameipongeza Taasisi ya Faraja Islamic Foundation kwa chini ya Mkurugenzi wake Hashim Madenge kwa kuona umuhimu wa kuandaa Mashindano ya Kuhifadhi Quran takatifu ambapo amesema Serikali itampatia ushirikiano sababu anachokifanya kina manufaa kwa wananchi.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »