MKURUGENZI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI KUSHTAKIWA KUTOWALIPA WENYEVITI WA MITAA

MKURUGENZI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI KUSHTAKIWA KUTOWALIPA WENYEVITI WA MITAA

Wenyeviti wa mitaa sitini na nane katika manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma wameazimia kuishtaki halmashauri hiyo kwa kushindwa kualipa stahiki zao kwa zaidi ya miezi minane na wengine kudai madai ya zaidi ya miaka minne. Ucheleweshwaji wa malipo ya madai hayo umefanya wenyekiti hao kukutana kujadili mustakabali juu ya malipo hayo ikiwemo kwenda mahakamani 

Wenyeviti wa mitaa sitini na nane katika manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma wameazimia kuishtaki halmashauri hiyo kwa kushindwa kualipa stahiki zao kwa zaidi ya miezi minane na wengine kudai madai ya zaidi ya miaka minne.

Ucheleweshwaji wa malipo ya madai hayo umefanya wenyekiti hao kukutana kujadili mustakabali juu ya malipo hayo ikiwemo kwenda mahakamani  kwani wenyeviti waliomaliza muda wao wanadai laki tisa na elfu arobaini kila mmoja huku walioko madarakani kwa sasa wakidai laki moja na elfu stini, na kwamba wamehangaika  kwa kipindi kirefu sana kudai posho hizo bila mafanikio licha ya kiwango hicho kuidhinishwa kisheria kama stahiki yao kwa kila mwezi.

Akitoa majibu juu ya madai hayo,mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma Ujiji MWAILWA PANGANI amekiri manispaa hiyo kudaiwa na kueleza tayari wameanza taratibu za tathmini.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »