Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel amesema kutokana na kuongezea kwa mahitaji ya upandikizaji wa viungo Nchini, Serikali imeandaa Muswada wa kutunga Sheria itakayoongoza taratibu za uvunaji, utunzaji na upandikizaji wa viungo. Ameeleza hayo akimjibu Mbunge wa Viti Maalum, Rose Tweve, aliyehoji kuhusu mkakati wa Serikali kuanzisha utaratibu maalum wa kuvuna viungo vya binadamu kama
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel amesema kutokana na kuongezea kwa mahitaji ya upandikizaji wa viungo Nchini, Serikali imeandaa Muswada wa kutunga Sheria itakayoongoza taratibu za uvunaji, utunzaji na upandikizaji wa viungo.
Ameeleza hayo akimjibu Mbunge wa Viti Maalum, Rose Tweve, aliyehoji kuhusu mkakati wa Serikali kuanzisha utaratibu maalum wa kuvuna viungo vya binadamu kama Figo na Moyo kwa ajili ya wenye uhitaji.
Naibu Waziri ameeleza, “Kwa kuwa huduma zimeanza kutolewa, kwa sasa Nchi inatumia miongozo ya kimataifa kusimamia uvunaji na upandikizaji wa viungo”.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *