Imeelezwa kuwa kuanzishwa kwa kiwanda cha Kusafisha Madinicha Mkoani Geita kitaongeza na kuchangamsha uchumi wa mkoana Taifa kwa ujumla wake.Waziri wa Madini Mhe Doto Biteko jana tarehe 8 Mei 2021 wakatiakiweka Jiwe la Msingi katika kiwanda cha kusafisha madini chaGGR akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Geita.Waziri Biteko amesema kuwa kiwanda hicho cha kisasa na
Imeelezwa kuwa kuanzishwa kwa kiwanda cha Kusafisha Madini
cha Mkoani Geita kitaongeza na kuchangamsha uchumi wa mkoa
na Taifa kwa ujumla wake.
Waziri wa Madini Mhe Doto Biteko jana tarehe 8 Mei 2021 wakati
akiweka Jiwe la Msingi katika kiwanda cha kusafisha madini cha
GGR akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Geita.
Waziri Biteko amesema kuwa kiwanda hicho cha kisasa na cha
kwanza cha aina yake barani Afrika kimekusudia kuimarisha nyanja
za kusafisha dhababu nchini jambo litakaloimarisha soko la
uhakika la uuzaji wa madini na kuiwezesha Benki kuu kununua
madini yenyewe.
Amesema kuwa ni fahari kubwa katika sekta ya madini kwani
uwekezaji huo ni mkubwa na muhimu utakaokijibu ndoto za
serikali katika kuwakomboa wachimbaji wadogo wa madini.
Mhe Biteko amewaasa wachimbaji kuwa na ushirikiano na
kupendana kwani uchumi wa nchi hauwezi kuimarika kwa baadhi
ya wachimabji kuwachukia waliofanikiwa.
“Nasikitika kuna vijiwe vimegawanyika kazi yao kusuka majuku na
kuwachukia wengine waliofanikiwa, Ushindeni ubaya kwa wema,
aliyefanikiwa tumuombee Mungu amsogeze mbele” Amekaririwa
Waziri Biteko
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Gabriel
Robert amesema kuwa dhahabu inayouzwa katika mkoa huo
imeamsha ari kwa wawekezaji kuanza kuwekeza katika sekta
mbalimbali jambo linaloimarisha uchumi wa mkoa.
Amesema kuwa mkoa wa Geita pamoja na mambo mengine lakini
ni sehemu sahihi kwa ajili ya kuwekeza katika sekta ya madini.
Awali akisoma taarifa ya kiwanda cha kusafisha madini cha GGR
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi Mhandisi Athuman Mfutakamba
amesema kuwa kiwanda hicho kilipewa leseni ya kusafisha
dhahabu No RFL 001/2019 iliyotolewa na Wizara ya Madini tarehe
16 Julai 2019 na kina uwezo wa kusafisha 400 kg kwa siku na
kufikia tani 200 kwa mwaka kwa kiwango cha juu kabisa na
kukidhi kufikia kiwango cha usafi wa asilimia 999.9 na 999.5
Amesema kampuni imejiimarisha ipasavyo kutekeleza wajibu huo
kwa kufunga vifaa/mashine za kusafisha dhahabu vya kisasa na
vyenye viwango vya hali ya juu vinavyokidhi viwango vya
kimataifa.
Na Mathias Canal, WazoHuru-Geita
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *