MAJALIWA: RAIS SAMIA AMETOA SH. BILIONI MBILI UJENZI WA MIRADI YA MAENDELEO NANGANGA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya Nanganga wilayani Ruangwa. Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Julai 4, 2022) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa kata hiyo akiwa