Dodoma JESHI la Polisi Mkoani Dodoma linawashikilia wahamiaji haramu 12 ambao ni raia wa Nchini Ethiopia Mmoja Kati yao anatokea Nchini Kenya. Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dodoma,Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa Raia hao wamekamatwa wiki iliyopita katika eneo la Wilaya ya Kongwa ambapo walikuwa wakichenji Dolla. Kamanda Muroto
Dodoma
JESHI la Polisi Mkoani Dodoma linawashikilia wahamiaji haramu 12 ambao ni raia wa Nchini Ethiopia Mmoja Kati yao anatokea Nchini Kenya.
Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dodoma,Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma,Gilles Muroto amesema kuwa Raia hao wamekamatwa wiki iliyopita katika eneo la Wilaya ya Kongwa ambapo walikuwa wakichenji Dolla.
Kamanda Muroto amesema kuwa Raia hao wenye asili ya Ethiopia walikuwa wamepakiwa kwenye Lori ambalo lilikuwa likiendeshwa na Dereva wa Kitanzania likielekea Nchini jirani ya Zambia ili kwenda Afrika ya Kusini.
Katika hatua nyingine,Kamanda Muroto amesema kuwa hali ya usalama Mkoani Dodoma imeendelea kuwa shwari wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi kutokana na kutokuwepo kwa vitendo vya kihalifu.
Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma kutofumbia macho vitendo vyote vya kihalifu bali wanapaswa kutoa taarifa kwa Jeshi hilo.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *