CCM YAIAGIZA SERIKALI KUFANYIA UPYA MAIPITIO YA SERA NA SHERIA ZA KODI

CCM YAIAGIZA SERIKALI KUFANYIA UPYA MAIPITIO YA SERA NA SHERIA ZA KODI

Na Barnabas Kisengi -Dodoma  CHAMA cha Mapinduzi kimeziagiza Serikali mbili ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Zanzibar kupitia ilani ya uchaguzi Ibara namba  18 na 20wakati maelekezo ya Rais yakifanyiwa kazi nazo zifanye upya mapitio ya  sera na Sheria za kodi  ili kuliweka  vyema suala hilo la tozo katika utekelezaji wake. Kauli hiyo imetolewa

Na Barnabas Kisengi -Dodoma 


CHAMA cha Mapinduzi kimeziagiza Serikali mbili ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Zanzibar kupitia ilani ya uchaguzi Ibara namba  18 na 20wakati maelekezo ya Rais yakifanyiwa kazi nazo zifanye upya mapitio ya  sera na Sheria za kodi  ili kuliweka  vyema suala hilo la tozo katika utekelezaji wake.

Kauli hiyo imetolewa hii leo Jijini Dodoma na Katibu wa itikadi na uenezi Shaka Hamdu Shaka wakati alipokuwa akizu gumza na waandishi wa habari.
Sanjari na hilo Chama hicho kimempongeza Rais Samia Sluhu Hassan ka hatua ya kusitisha tozo ya miamala ya simu kwa lengo la kuwajali wananchi maskini.


Aidha katika hatua nyingine chama hicho kimempongeza  Sheha Mpemba  Faki kuwa Mbunge wa Jimbo la Konde Wilaya ya Micheweni Zanzibar baada ya kushinda uchaguzi Uliofanyika Julai 18 Mwaka huu ambaye  alipata kura 1796  huku mgombea Mwenzie Mohamed Issa wa Chama cha ACT Wazalendo akipata kura 1373.

Hata hivyo katibu huyo amesema kuwa Chama Chama cha Mapinduzi (CCM )kimejipambanua katika Ilani yake ya uchaguzi ya Mwaka 2020/2025 kuhakiksha inawaletea wananchi maendeleo.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »