Na Barnabas Kisengi, DODOMA KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kenan Kihongosi amemvaa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) John Pambalu kwa kumtaka kuwa na adabu na kuheshimu sheria za Nchi huku akiwataka watanzania kutoandamana Julai 5 mwaka huu. Hatua hii imekuja
Na Barnabas Kisengi, DODOMA
KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kenan Kihongosi amemvaa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) John Pambalu kwa kumtaka kuwa na adabu na kuheshimu sheria za Nchi huku akiwataka watanzania kutoandamana Julai 5 mwaka huu.
Hatua hii imekuja kufuatia Mwenyekiti huyo wa Bavicha kutoa tamko kuwataka Vijana wa Chama hicho kuandamana Agosti 5 kwa madai ya kudai demokrasia kuhusu kesi inayomkabili Mwenyekiti wao Freeman Mbowe.
Akizungumza leo Agosti 3,2021,Katibu Mkuu huyo wa UVCCM amesema kuwa ni aibu kwa watu wazima kuendelea kung’ang’ania mambo ambayo hayawezekani huku akiwataka kufuata taratibu za mahakama ambapo amedai hakuna mtu aliye juu ya sheria na hakuna mwenye mamlaka ya kumtaka Mheshimiwa Rais kufanya jambo au matakwa yao binafsi.
Katibu huyo ameeleza kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA lazima atambue kwamba nchi hii inaongozwa na Sheria na kwamba siku zote wao wamekuwa wakijipambanua kuwa wanataka Demokrasia Sasa anashangaa wanataka kuvunja Sheria na kusahau kuwa kila mhimili unafanya kazi kwa namna yake.
“Mnapotaka kuandamana kupinga kuhusu yanayomhusu Mbowe mmejiridhisha vipi kwamba hana makosa,mna wajibu wa kutii sheria za nchi,”amesema.
Kihongosi amewataka Wanachama hao wanaotaka kuandamana kuendelea kufanya shughuli za Maendeleo kwa ajili ya manufaa kwa familia zao badala ya kutumia muda huo kwa masuala yasiyo na msingi.
“Niwashauri tu vijana wenzangu, badala ya kuandamana muda huo tumieni kutafuta ugali wa familia zenu.Wapinzani wanapaswa wajitafakari ,wabadilike na kukubali kubadilisha aina ya Mfumo wa siasa wanaoutumia ,lazima katika siasa kuna ushindani,wahakikishe wanakuwa Mabalozi wa amani na kuepuka kuhamasisha vurugu,”amesema.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *