Mahakama ya wilaya ya Kigoma imemuhukumu Agness Damian( 40)mkazi wa Mji mwema manispaa ya Kigoma Ujiji kwenda jela miaka miwili na kulipa fidia ya shilingi milioni tano kwa kosa la kumshambulia na kumkatakata kwa wembe mtoto wa mme wake mwenye umri wa miaka 15. Kesi namba 95 ya mwaka 2020 dhidi ya Agness Damian inadaiwa
Mahakama ya wilaya ya Kigoma imemuhukumu Agness Damian( 40)mkazi wa Mji mwema manispaa ya Kigoma Ujiji kwenda jela miaka miwili na kulipa fidia ya shilingi milioni tano kwa kosa la kumshambulia na kumkatakata kwa wembe mtoto wa mme wake mwenye umri wa miaka 15.
Kesi namba 95 ya mwaka 2020 dhidi ya Agness Damian inadaiwa kosa hilo alilitenda mnamo 18 June,2020 baada ya mwanamke huyo kumtuhumu aliyejeruhiwa na tukio hilo kuwa amempiga mdogo wake ambaye ni mtoto wake
Inaelezwa mshtakiwa alitekeleza ukatili huo na kumsababisha muhanga kupata majeraha na kulazwa hospitali kwa siku nane akifanyiwa matibabu
Eva Mushi hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya kigoma amesema mahakama imepitia na kuridhishwa na ushahidi upande wa mashtaka uliojumuisha mhanga wa tukio hilo,mama mzazi wa mtoto na baba mzazi wa mtoto huyo ,jirani ,Daktari na ushahidi wa polisi.
Hivyo mahakama imemtia hatihani kwa mujibu wa kifungu cha 225 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 marejeo ya mwaka 2019 mahakama imemtia hatiani na kumuhukumu kwenda jela miaka miwili na fidia ya milioni tano.
kabla ya hukumu mshtakiwa alipotakiwa kujitetea aliomba mahakama impunguzie adhabu kwani yeye ni yatima na anategemewa na watoto wawili na kati yao mmoja akiwa na umri mdoogo
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *