EWURA YATANGAZA KUPANDA KWA BEI ZA MAFUTA KUANZIA SEPTEMBA 01, 2021

EWURA YATANGAZA KUPANDA KWA BEI ZA MAFUTA KUANZIA SEPTEMBA 01, 2021

Na Barnabas Kisengi-Dodoma  Mamlaka ya Uthibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kupanda kwa bei za mafuta nchini kuanzia Semptemba 01 2021 kwa bei za mafuta ya petroli, Dizeli na mafuta ya taa Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Mkuu wa kitengo cha  mahusiano na habari Titus Kaguo amesema kuwa Ewura imetangaza kupanda kwa

Titus Kaguo, Mkuu wa Kitengo cha  Mahusiano na Habari-EWURA

Na Barnabas Kisengi-Dodoma 


Mamlaka ya Uthibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kupanda kwa bei za mafuta nchini kuanzia Semptemba 01 2021 kwa bei za mafuta ya petroli, Dizeli na mafuta ya taa


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Mkuu wa kitengo cha  mahusiano na habari Titus Kaguo amesema kuwa Ewura imetangaza kupanda kwa bei hizo za mafuta kuanzia septemba 01 2021 hapa nchini. 


Kaguo amesema kwa Bandari ya Dar es Salaam  bei imepanda kwa mafuta ya petroli Tsh 84, dizeli Tsh 39 na mafuta ya taa Tsh 18 na kwa bandari Tanga petroli ni Tsh 53, dizeli 14 na kwa bandari ya Mtwara petroli imepanda kwa Tsh 108 na dizeli imepanda kwa Tsh 46
Aidha kaguo amesema bei hiyo ndiyo itaanza kutumika kesho na amewataka wananchi wanaotumia nishati ya mafuta kuhakikisha hawauziwi zaidi ya bei iliyoelekezwa na EWURA na pindi watakapoona bei imezidi watoe taarifa kwa vyombo husika. 

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »