RC MAKALLA ATATUA MIGOGORO YA WANANCHI JIMBO LA MBAGALA.

RC MAKALLA ATATUA MIGOGORO YA WANANCHI JIMBO LA MBAGALA.

>>Aweka rekodi ya kusikiliza kero hadi majira ya usiku. >>Taa na torch za simu zatumika kuongeza mwanga.- >>Ni utekelezaji wa ahadi ya kusikiliza kila aliewasilisha kero. >>Wananchi wakoshwa na zoezi la Utatuzi wa kero. >>Awataka Watendaji kutatua kero za Wananchi kuanzia ngazi ya Mitaa. Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amelazimika

>>Aweka rekodi ya kusikiliza kero hadi majira ya usiku.

>>Taa na torch za simu zatumika kuongeza mwanga.-

>>Ni utekelezaji wa ahadi ya kusikiliza kila aliewasilisha kero.

>>Wananchi wakoshwa na zoezi la Utatuzi wa kero.

>>Awataka Watendaji kutatua kero za Wananchi kuanzia ngazi ya Mitaa.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amelazimika kusikiliza na kutatua Migogoro ya kila mwananchi aliewasilisha kero yake kwenye mkutano wake Jimbo la Mbagala ili kuhakikisha kila aliewasilisha kero anasikilizwa na kupata ufumbuzi.

Uamuzi wa RC Makalla kusikiliza Migogoro ya Wananchi hadi majira ya usiku ni Kufuatia mwitikio mkubwa wa Wananchi waliowasilisha kero zao.

Mkuu wa Mkoa wa Dar ES Salaam, Mhe. Amos Makalla akiongea na Wananchi wa Jimbo la Mbagala Mara baada ya kusikiliza Kero zao.

RC Makalla amefanikiwa kusikiliza na kutatua Mamia ya Migogoro ya Wananchi waliowasilisha ambapo Migogoro iliyoonekana kuhitaji ufuatiliaji wa kina amezikabidhi idara husika kwaaajili ya utatuzi.

Miongoni mwa kero zilizowasilishwa ni Migogoro ya ardhi, Ubovu wa Barabara, Mirathi, Biashara holela, Dhuluma, kero ya Maji na Migogoro mingine.

Wananchi wa Jimbo la Mbagala waliojitokeza kuwasilisha Kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar ES Salaam Mhe Amos Makalla

Aidha RC Makalla ameamuru kuondolewa kwa watu wote wanaofanya biashara ndani ya eneo la Ujenzi wa Barabara ya Mwendokasi eneo la Mbagala Rangi tatu kwakuwa inahatarisha usalama wao na kumzuia Mkandarasi kufanya majukumu yake.

Hata hivyo RC Makalla amezielekeza Taasisi zote zinazomiliki Maeneo Makubwa ya ardhi kuhakikisha wanayalinda na Kuyaendeleza kwakuwa yamekuwa chanzo Cha tatizo la Migogoro ya Uvamizi wa Ardhi.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla kesho September 03 ataendelea na ziara yake ya kusikiliza na kutatua Migogoro ya Wananchi wa Jimbo la Kigamboni kuanzia saa mbili Asubuhi Hadi Jioni.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »