WIZARA YA AFYA YATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU

WIZARA YA AFYA YATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU

Na Barnabas Kisengi, Dodoma  WIZARA ya Afya,Maendeleo ya Jamaii Jinsia Wazee na Watoto imetekeleza maagizo ya Waziri Mkuu Kasim Majaliwa  aliyoyatoa Mkoani Katavi Agosti 27 Mwaka huu alipotembelea Hospitali ya Mkoa huo. Akizungumza na Waandishi wa Habari,hii leo Jijini Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Profesa Abel Makubi kuhusiana na maagizo hayo amesema kuwa miongoni mwa

Na Barnabas Kisengi, Dodoma 

WIZARA ya Afya,Maendeleo ya Jamaii Jinsia Wazee na Watoto imetekeleza maagizo ya Waziri Mkuu Kasim Majaliwa  aliyoyatoa Mkoani Katavi Agosti 27 Mwaka huu alipotembelea Hospitali ya Mkoa huo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari,hii leo Jijini Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Profesa Abel Makubi kuhusiana na maagizo hayo amesema kuwa miongoni mwa maagizo hayo ni pamoja na  Wizara ya Afya kutakiwa irudishe usimamizi wa mradi  wa ujenzi wa Hopsitali ya Mkoa huo kwa Katibu Tawala Mkoa wa Katavi.

Amesema maagizo mengine ni Katibu Tawala mkoa wa Katavi kutakiwa aunde kamati zitakazowezesha utekelezaji wa ujenzi wa jengo la Hospitali ya Mkoa pamoja na fedha za utekelezaji wa mradi kiasi cha sh Milioni 688 zihamishiwe kwa katibu tawala wa Mkoa wa Katavi.

Hata hivyo Profesa Makubi ameeleza kuwa  katika kuhakikisha Hospitali  hiyo inakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi bila kuchelewa,Wizara  imeshaandaa mahitaji halisi ya vifaa,samani,TEHAMA na wataalam ,mchakato  wa upatikanaji wa vifaa hivyo umeshaanza.

Pia amesema kutokana na umuhimu wa kuzishirikisha Ofsi za Wakuu wa Mikoa katika utekelezaji wa miradi hiyo kuna umuhimu kwa jamii kuanzia sasa  kushiriki kikamilifu katika miradi hiyo.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »