Mkurugenzi Idara ya Uratibu Shughuli za Serikali Ndugu Siajabu Sleiman Pandu amewataka washiriki wa Miradi ya ajira za muda kuyatumia vyema Mafunzo waliyoyapata ili kufanikisha lengo lililokusudiwa. Mkurugenzi Sijaabu amesema hayo katika Ukumbi wa Betres Nkurumah wakati wa akiyafunga rasmi Mafunzo ya siku tatu yaliyowashirikisha wawezeshaji kutoka shehia mbali mbali za Unguja ambapo amewataka kuwa
Mkurugenzi Idara ya Uratibu Shughuli za Serikali Ndugu Siajabu Sleiman Pandu amewataka washiriki wa Miradi ya ajira za muda kuyatumia vyema Mafunzo waliyoyapata ili kufanikisha lengo lililokusudiwa.
Mkurugenzi Sijaabu amesema hayo katika Ukumbi wa Betres Nkurumah wakati wa akiyafunga rasmi Mafunzo ya siku tatu yaliyowashirikisha wawezeshaji kutoka shehia mbali mbali za Unguja ambapo amewataka kuwa makini kwa kutoa taarifa sahihi za Walengwa kutokana na umuhimu wake katika kufanikisha mipango ya serikali.
Amesema taarifa hizo zitasaidia kupunguza malalamiko kwa Walengwa watakaoibuliwa katika kutekeleza ajira za muda katika Sheiha zao.
Nae, Mratibu wa Tasaf Zanzibar Saida Salehe amewataka washiriki hao kufanye kazi kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa kwani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajia matokeo yatakayo leta tija katika utekelezaji wa Miradi hiyo
Nao washiriki wa Mafunzo hayo wameushukuru uwongozi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais kwa kuwaandalia Mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyia kazi mafunzo kama inavo tarajiwa.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *