TAASISI YA MAENDELEO YA JAMII TENGERU NI MFANO KATIKA TAALUMA: DKT. ROSEMARY MWAIPOPO

TAASISI YA MAENDELEO YA JAMII TENGERU NI MFANO KATIKA TAALUMA: DKT. ROSEMARY MWAIPOPO

Na Mwandishi Maalum Tengeru Arusha Inaelezwa kuwa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru ni moja ya Taasisi muhimu katika kuleta mabadiliko katika kuleta maendeleo nchini ikiwa ni sehemu inayozalisha wataalam wa Maendeleo ya Jamii wanaotumika kutatua changamoto katika jamii. Hayo yamebainika leo mkoani Arusha katika Kongamano la kitaaluma lililofanyika katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii

Na Mwandishi Maalum Tengeru Arusha

Inaelezwa kuwa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru ni moja ya Taasisi muhimu katika kuleta mabadiliko katika kuleta maendeleo nchini ikiwa ni sehemu inayozalisha wataalam wa Maendeleo ya Jamii wanaotumika kutatua changamoto katika jamii.

Hayo yamebainika leo mkoani Arusha katika Kongamano la kitaaluma lililofanyika katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii kuelekea Mahafali ya 11 ya Taasisi hiyo.

Akizungumza katika Kongamano hilo Mwenyekiti wa Bodi ya uendeshaji wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt. RoseMary Mwaipopo amesema Taasisi hiyo amesema wahitimu wa Taaluma ya Maendeleo ya Jamii wanatakiwa kutumia ujuzi wao katika kusaidia kutatua changamoto na kuchagiza katika fursa mbalimbali.

Dkt. Rosemary amewataka wahitimu wa Taasisi hiyo kujitathimini ni nini wanaweza kufanya katika kuisaida jamii inayowazunguka hasa katika kuhakikisha wanatafuta namana sahihi ya kutumia fursa zilizopo kutatua changamoto za ajira.

“Naomba mjitathimini mkalete mabadiliko katika jamii mkatumie elimu mliyoipata hapa mlete matokeo chanja kwaajili ya amendeleo ya jamii ” alisema Dkt. Rosemary

Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru Dkt. Bakari George ameeleza kuwa wahitimu kutoka katika Taasisi hiyo wanatakiwa kutumia teknolojia iliyopo kama fursa ya kutafuta namna ya kupata ajira au kujiajiri katika sekta mbalimbali.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Extended Impression Paul Patrick amesema kuwa wahitimu wa Vyuo wanatakiwa kuwa na udhubutu wa kufanya mabadiliko katika jamii kwa kuajiriwa na kujiajiri ili kutatua changamoto zilizopo katika jamii.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »