Kwa upande wa Kidato cha Kwanza mwaka 2022 jumla ya wanafunzi 907,803 wakiwemo wavulana 439,836 na wasichana 467,967 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2021 ikilinganishwa na wanafunzi 833,872 waliojiunga kidato cha kwanza 2021. Wanafunzi hao wanatarajiwa kuanza masomo tarehe 17 Januari, 2022 na orodha yao tayari imekwishatolewa ikionesha shule wanazotakiwa kusoma. Uchambuzi unaonesha
Kwa upande wa Kidato cha Kwanza mwaka 2022 jumla ya wanafunzi 907,803 wakiwemo wavulana 439,836 na wasichana 467,967 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2021 ikilinganishwa na wanafunzi 833,872 waliojiunga kidato cha kwanza 2021.
Wanafunzi hao wanatarajiwa kuanza masomo tarehe 17 Januari, 2022 na orodha yao tayari imekwishatolewa ikionesha shule wanazotakiwa kusoma.
Uchambuzi unaonesha kuwa Mikoa 5 yenye matarajio ya kupokea wanafunzi wengi zaidi kwa Kidato cha Kwanza ni Dar es Salaam (78,738), Mwanza (68,725), Kagera (50,735), Mara (48,855) na Morogoro (48,515).
Jumla ya wanafunzi wanaotarajiwa kuandikishwa shuleni kwa mwaka wa masomo 2022 ili waanze masomo Januari, 2022 ni 3,853,460, hii ikiwa ni wanafunzi wa Darasa la Awali 1,363,834; Darasa la Kwanza 1,581,823 na Kidato cha Kwanza 907,803, ikilinganishwa na wanafunzi 3,631,715 wakiwemo wanafunzi 1,198,564 wa darasa la Awali, wanafunzi 1,549,279 wa darasa la Kwanza na wanafunzi 883,872 wa Kidato cha Kwanza 2021.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *