NSSF WATOA MSAADA WA VIFAA TIBA KATIKA HOSPITALI YA MNAZI MMOJA ZANZIBAR

NSSF WATOA MSAADA WA VIFAA TIBA KATIKA HOSPITALI YA MNAZI MMOJA ZANZIBAR

NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF )Tanzania Bara umetoa Msaada wa Vifaa Tiba ikiwemo Vitanda na Mashine kwa ajili ya kupima Shinikizo la damu kwa wagonjwa wanaopata matibabu katika Hospitali ya Mnazi mmoja iliyopo Visiwani Zanzibar ikiwa ni sehemu ya kuwajibika katika jamii. Katika kutoa msaada huo NSSF ilisindikizwa

NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF )Tanzania Bara umetoa Msaada wa Vifaa Tiba ikiwemo Vitanda na Mashine kwa ajili ya kupima Shinikizo la damu kwa wagonjwa wanaopata matibabu katika Hospitali ya Mnazi mmoja iliyopo Visiwani Zanzibar ikiwa ni sehemu ya kuwajibika katika jamii. Katika kutoa msaada huo NSSF ilisindikizwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kutoka na utendaji wa mashirikiano uliopo katika Mifuko hii.

Meneja uhusiano na Elimu kwa Umma – NSSF Lulu Mengele

Katika kuelekea Siku ya Wanamke Duniani Marchi 8 akizungumza leo na waandishi wa Habari, Meneja uhusiano na Elimu kwa Umma – NSSF Lulu Mengele kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF amesema Jukumu la kusaidia ni sehemu ya kuwajibika katika Jamii kwa kutoa misaada na kwa kutambua thamani ya mwanamke katika Jamii wameamua kutoa msaada wa vifaa tiba katika hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar. Wakati wa kutoa msaada huo NSSF imesindikzwa na ZSSF kwa lengo la kukuza mashirikiano baina ya Mifuko hii.

Afisa utawala ZSSF, Nassor Hassan

Naye Afisa utawala ZSSF Nassor Hassan katika tukio hilo ameishukuru uongozi wa hospitali hiyo kwa kuwapokea huku akieleza ushirikiano walionao na NSSF.

Dkt. Msafiri Marijani Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar

             Dkt. Msafiri Marijani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar baada ya kupokea Msaada huo wa Vifaa Tiba ameishukuru NSSF kwa msaada huo na kueleza uhitaji walionao katika hispitali hiyo.

Violet Segeja Mwenyekiti wa Wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii NSSF

Violet Segeja ni Mwenyekiti wa Wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii NSSF katika tukio hilo ametoa wito kwa Jamii hasa wanawake walio katika Vikundi kujiandikisha katika sekta isiyo rasmi katika Mifuko kwa ajili ya manufaa yao ya Baadaye.

Mkuu wa Mfuko wa uchangiaji  Hiyari – ZSSF Rajabu Haji Machano

Kwa upande wake Mkuu wa Mfuko wa uchangiaji  Hiyari – ZSSF Rajabu Haji Machano pamoja na kutoa shukrani kwa mashirikiano na NSSF ametoa wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Hiari.

Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja  Zanzibar ni hospitali  inayotegemewa na idadi kubwa ya Wananchi hivyo kutolewa kwa msaada huo kutoka NSSF itakuwa ni sehemu ya kuisaidia Jamii kubwa kupata huduma bora zaidi.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »