Mfano wa hundi ikikabidhiwa kwa Mabingwa wa NBC Premier League msimu huu wa 2021/2022, Young Africans SC, na kupokelewa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Senzo Hammilton Mazingiza “Mbatha” Zawadi kwa timu zilizofanya vizuri NBC Premier League na Ligi Kuu ya Wanawake (Serengeti Light Women’s Premier League 2021|2022) LIGI KUU YA WANAWAKE1.Simba Queens [Bingwa]2.Fountain Gate Princess
Mfano wa hundi ikikabidhiwa kwa Mabingwa wa NBC Premier League msimu huu wa 2021/2022, Young Africans SC, na kupokelewa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Senzo Hammilton Mazingiza “Mbatha”
Zawadi kwa timu zilizofanya vizuri NBC Premier League na Ligi Kuu ya Wanawake (Serengeti Light Women’s Premier League 2021|2022)
LIGI KUU YA WANAWAKE
1.Simba Queens [Bingwa]
2.Fountain Gate Princess (Mshindi wa Pili)
3.Yanga Princess (Mshindi wa Tatu)
NBC PREMIER LEAGUE
1.Yanga SC (Bingwa)
2.Simba SC (Mshindi wa Pili)
3.Azam FC (Mshindi wa Tatu)
4.Geita Gold FC (Mshindi wa Nne)
Tuzo ya Kocha Bora NBC Premier League msimu 2021/2022 imekwenda kwa Kocha wa Young Africans SC SC, Nasreddine Nabi ambaye amewakilishwa na msaidizi wake Cedric Kaze.
Tuzo ya Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya NBC 2021/2022 imekwenda kwa Mshambuliaji wa Geita Gold FC, George Mpole aliyemaliza msimu na mabao 17.
Tuzo ya beki Bora wa Ligi Kuu ya NBC 2021/2022 imekwenda kwa Hennock Inonga wa Simba SC, na Aishi Manula ameipokea kwa niaba yake.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa NBC Premier League msimu huu wa 2021/2022 imekwenda kwa Yannick Bangala wa Yanga SC, na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa timu hiyo Senzo Hammilton Mazingiza “Mbatha” akaipokea kwa niaba yake.
Tuzo ya Kiungo Bora wa NBC Premier League msimu huu wa 2021/2022 imekwenda kwa Yannick Bangala naye Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga SC, Thabithy Kandoro ameipokea kwa niaba yake.
Tuzo ya Goli Bora kwenye NBC Premier League msimu huu imekwenda kwa Fiston Mayele wa Yanga SC vs Biashara United FC, na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa timu hiyo Senzo Hammilton Mazingiza “Mbatha” akaipokea kwa niaba yake.
Tuzo ya Golikipa Bora wa NBC Premier League imekwenda kwa Djigui Diarra wa Yanga SC, naye Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga SC, Thabithy Kandoro ameipokea kwa niaba yake.
Tuzo ya Mfungaji Bora wa Azam Sports Federation Cup 2021/2022 imekwenda kwa Kiungo mshambuliaji wa Coastal Union FC Abdul Suleiman ‘Sopu’ aliyemaliza na mabao 09.
Tuzo ya timu yenye nidhamu msimu wa 2021/2022 imekwenda Tanzania Prisons FC ya Mbeya.
Moja ya Tuzo za Heshima za Rais wa TFF imekwenda kwa Kocha wa Serengeti Girls, Bakari Shime ambaye ameiwezesha timu hiyo kwenda Kombe la Dunia.
Tuzo ya Mwamuzi Bora NBC Premier League 2021/2022 imekwenda kwa Ahmed Arajiga.
Tuzo ya Kocha Bora Ligi Kuu ya Wanawake (Serengeti Light Women’s Premier League 2021/2022) imekwenda kwa Sebastian Nkoma wa Simba Queens.
Tuzo ya Kipa Bora wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Lite 2021/2022 imekwenda kwa Gelwa Yona wa Simba Queens.
Tuzo ya Kipa Bora wa Azam Sports Federation Cup 2021/2022 ni Mohamed Mohamed wa Coastal Union FC
Mchezaji Bora Chipukizi wa NBC Premier League 2021/2022 ni Dickson Mhilu wa Kagera Sugar FC
Mchezaji Bora Chipukizi wa Serengeti Light Women’s Premier League 2021/2022 ni Clara Luvanga wa Yangasc Princess.
KIKOSI Bora cha Msimu NBC Premier League 2021/2022
1:Djigui Diarra – Yanga SC
2:Djuma Shabani – Yanga SC
3:Mohamed Hussein – Simba SC
4:Hennock Inonga – Simba SC
5:Bakari Mwamnyeto – Yanga SC
6:Yanick Bangala – Yanga SC
7:Abdul Hamis Suleiman – Coastal Union FC
8:Feisal Salum – Yanga SC
9:Fiston Mayele – Yanga SC
10:George Mpole – Geita Gold FC
11:Pape Ousmane Sakho – Simba SC
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *