MWANDISHI WA HABARI AJITOSA KINYANG’ANYIKO CCM

MWANDISHI WA HABARI AJITOSA KINYANG’ANYIKO CCM

Na Barnabas Kisengi-Dodoma Mwandishi wa Habari wa kituo cha Upendo Tv Mkoani Dodoma Bi Doreen Aloyce  amejitokeza katika Ofisi za Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Dodoma kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Ujumbe wa NEC Taifa. Bi Doreen Aloyce  amesema ameamua kuchukua fomu hiyo ya kuwania nafasi ya mjumbe wa NEC Taifa baada ya

Na Barnabas Kisengi-Dodoma


Mwandishi wa Habari wa kituo cha Upendo Tv Mkoani Dodoma Bi Doreen Aloyce  amejitokeza katika Ofisi za Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Dodoma kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Ujumbe wa NEC Taifa.


Bi Doreen Aloyce  amesema ameamua kuchukua fomu hiyo ya kuwania nafasi ya mjumbe wa NEC Taifa baada ya kujitathimini kuwa anaweza na ana uwezo huo wa kukitumikia chama cha Mapinduzi CCM katika nafasi hiyo ya kuwa mjumbe wa NEC Taifa.
“Nimeona ninatosha na nina uwezo mkubwa katika nafasi hii muhimu katika chama changu kwa kuweza kumsaidia Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi Taifa ambaye pia ni RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA SAMIA SULLUH HASSAN katika utendaji wake wa majukumu katika Chama cha Mapinduzi CCM na kwakuwa Chama chetu kwa sasa ndicho kinaisimamia serikali, hivyo kwa uwezo wangu nina hakika nitafanya vizuri”amesema Doreen Aloyce.


Aidha Mwandishi huyo amesema kuwa anaitumia haki yake ya kikatiba ya Chama chake kuwa huru kugombea nafasi yote aitakayo katika chama chake katika nafasi yoyote.”.                       pia nikiangalia nimekuwa ndani ya chama changu kwa muda mrefu kuanzia ngazi ya chipukizi, umoja wa vijana hadi sasa ambapo nimejiona ninatosha kuwania nafasi hii ya ujumbe wa NEC Taifa.”


Aidha Bi Dorin Aloicey amewasisitiza wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM na wasio kuwa wanacha wa Chama hicho kuhakikisha wanajitokeza Katika zoezi la SENSA ya watu na makazi ili kuisaidia Serikali kuwa na twakwakimu sahihi ya wananchi wake ili serikali inapokuwa inapanga mipango ya Maendeleo iweze kuwafikia Wananchi wote hapa nchini.
Mchakato Huu  wa uchaguzi ndani ya chama cha mapinduzi CCM ,ambao unafanyika kila baada ya miaka mitano kwa ajili ya kuchagua viongozi mbalimbali wa chama kuanzia ngazi ya mashina, matawi, wilaya,mkoa na jumuiya zake katika ngazi zote hadi Taifa unaendelea kwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM hapa nchini.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »