WAZIRI MKUU ATOA AGIZO WASIMAMIZI MJI WA SERIKALI.

WAZIRI MKUU ATOA AGIZO WASIMAMIZI MJI WA SERIKALI.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimpa zawadi Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, Hyeong Ryeol Kim alipozungumza naye kwenye Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam, Januari 26, 2024  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimpa zawadi Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, Hyeong Ryeol Kim alipozungumza naye kwenye Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam, Januari 26, 2024 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, alipozungumza naye kwenye Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam, Januari 26, 2024

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, Hyeong Ryeol Kim alipozungumza naye kwenye Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam, Januari 26, 2024 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wasimamizi na wataalamu wa ujenzi wa Mji wa Serikali jijini Dodoma wahakikishe matarajio ya ujenzi huo yanafikiwa kama ilivyokusudiwa.

Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na Mtawala wa Mamlaka ya Kusimamia Uendelezaji wa Mji wa Serikali wa Korea Kusini, Mheshimiwa HyeongRyeol Kim.

Amekutana na kiongozi huyo leo Ijumaa, Januari 26, katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni Jijini Dar es Salaam, baada ya hafla ya utiaji saini mikataba ya makubaliano kati ya taasisi za Korea Kusini na Tanzania.

Makubaliano hayo yanahusu kubadilishana uzoefu juu ya usimamizi na uratibu wa uendelezaji wa makao makuu na mji wa Serikali pamoja masuala ya ujenzi vikiwemo viwanda, hoteli.

Utiwaji saini huo umefanyika kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi Uendelezaji wa Mji wa Segong na kampuni ya Heerim ya Korea Kusini katika masuala ya usanifu na ubunifu wa ujenzi kwenye Mji wa Serikali na Makao Makuu jijini Dodoma.

“Serikali ya Tanzania na Korea Kusini zina mahusiano mazuri ya kidiplomasia, hivyo matarajio yetu ni kuona Makao Makuu na Mji wa Serikali jijini Dodoma unakuwa mzuri.”

Kwa upande wake, Mheshimiwa HyeongRyeol Kim amesema utiaji saini wa makubaliano hayo ni fursa muhimu ya kuendeleza ushirikiano baina ya mataifa hayo.

Pia, Mheshimiwa Kim amemshukuru Waziri Mkuu kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na amemuhakikishia kwamba nchi yao itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuliendeleza jiji la Dodoma.

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Translate »