Na Mwandishi wetu , MBEYA KIJANA Ivan Kabambala mwenye umri wa miaka (17) Mkazi wa Kagera katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya baada ya kudaiwa kupigwa risasi mgongoni na Askari wa Jeshi la Polisi. Akizungumzia tukio hilo, baba mzazi wa marehemu, Aggrey Kabambala,
Na Mwandishi wetu , MBEYA
KIJANA Ivan Kabambala mwenye umri wa miaka (17) Mkazi wa Kagera katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya baada ya kudaiwa kupigwa risasi mgongoni na Askari wa Jeshi la Polisi.
Akizungumzia tukio hilo, baba mzazi wa marehemu, Aggrey Kabambala, amesema limetokea majira ya saa mbili usiku katika eneo ambalo marehemu alikuwa anafanya kazi ya kuosha magari
Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Kagera wamelalamikia kitendo hicho na kudai kuwa Jeshi la Polisi linahatarisha usalama wao.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntinika ametoa pole kwa familia ya marehemu Ivan na kuwaomba wananchi wa Mtaa wa Kagera kuwa watulivu wakati wakisubiri ukweli wa tukio hilo.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, amesema marehemu Ivan ni miongoni mwa vijana 20 waliokuwa wakipanga njama za kufanya uhalifu na kwamba baada ya kupata taarifa Jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio.
Leave a Comment
Your email address will not be published. Required fields are marked with *