RAIS DK.HUSSEIN MWINYI AKUTANA NA DR.FAUSTINE NDUGULILE

RAIS DK.HUSSEIN MWINYI AKUTANA NA DR.FAUSTINE NDUGULILE

STATE HOUSE ZANZIBAR OFFICE OF THE PRESS SECRETARY PRESS RELEASE   Zanzibar                                                        11.03.2021 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameeleza haja kwa Wizara ya Mawasiliano ya Teknolojia ya Habari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushirikiana na Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

  Zanzibar                                                        11.03.2021

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameeleza haja kwa Wizara ya Mawasiliano ya Teknolojia ya Habari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushirikiana na Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa azma ya kupeana uzoefu.

Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo leo Ikulu Jijini Zanzibar wakati alipokutana na Waziri wa  Wizara ya Mawasiliano ya Teknolojia ya Habari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk. Faustine Engelbert Ndugulile pamoja na ujumbe wake waliofika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha kwa Rais na kuitambulisha Wizara hiyo mpya.

Katika maelezo yake, Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Mashirikiano kwa Wizara hizo mbili yanahitajika hasa ikizingatiwa kwamba Zanzibar  nayo ingependa kwenda kwa kasi katika sekta hiyo Teknolojia ya Habari hivi sasa.

Rais Dk. Mwinyi alieleza kwamba juhudi za makusudi zitaendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha malengo yaliyowekwa katika kuimarisha teknolojia ya habari hapa nchini yanafikiwa kwa mashirikiano ya pamoja kati ya Wizara hizo mbili.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi alimkaribisha Waziri huyo na Ujumbe wake Zanzibar na kumpongeza kwa kufika Zanzibar akiwa na ujumbe wake kwa ajili ya kujitambulisha sambamba na kukutana na uongozi wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Nae Waziri wa  Wizara ya Mawasiliano ya Teknolojia ya Habari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dk. Faustine Engelbert Ndugulile alianza kwa kumpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kuchaguliwa kwa kishindo na wananchi wa Zanzibar na kuonesha imani kubwa kwake.

Katika maelezo yake Waziri Ndugulile alisema kuwa Wizara hiyo imeanzishwa tarehe 5,  Disemba 2021 katika maandalizi ya kuiandaa nchi kwenda katika uchumi wa kidijitali na Mapinduzi ya Viwanda sambamba na kutengeneza Serikali ya Kimtandao na biashara Mtandao pamoja na sekta hiyo kuweza kuwa na mchango katika pato la Taifa.

Alisema kwamba kwa msingi huo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli aliona ni muhimu kuwa na Wizara ambayo itakuwa inashughulikia Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Aliongeza kuwa kwa vile baadhi ya majukumu ya Wizara hiyo ni ya Muungano hivyo amekuja  Zanzibar na ujumbe wake na kufanya mikutano ya mashirikiano na Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo pia, alifanya ziara kisiwani Pemba kwa ajili ya kuvitembelea vituo vya Tehama.

Alisema kuwa kikao chao na Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kimekwenda vizuri na ana matumaini makubwa kwamba mafanikio makubwa zaidi yatafikiwa huku akieleza azma ya ziara yake aliyoifanya kwa upandewa Unguja na Pemba.

Alisema kuwa kuhusu mradi wa anuani za makaazi ambao unatekelezwa hapa Zanzibar wameamua kuuengezea kasi ambao umeanza kwa ngazi za majaribio hasa kwa Zanzibar kutokana na kuimarika sekta ya Utalii hivyo, ni vizuri mitaa ikawa na majina na majengo yakawa na namba ili kuweza kufikika kirahisi na mradi huo kuwa na tija zaidi sanjari na kurahisisha biashara mtandao.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »