SPIKA AONGOZA WAKAZI WA DODOMA KUOMBOLEZA KIFO CHA RAIS MAGUFULI

SPIKA AONGOZA WAKAZI WA DODOMA KUOMBOLEZA KIFO CHA RAIS MAGUFULI

Na Saleh Ramadhani–Dodoma Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai amesema wao kama mhimili  wa Bunge wamepokea kwa masikitiko makubwa kuhusiana na kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Dkt.John  Pombe Magufuli ambapo amesema ni pigo kubwa kwa Watanzania kwani alikuwa shupavu  na mpambanaji. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 18,2021

Na Saleh RamadhaniDodoma

Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai amesema wao kama mhimili  wa Bunge wamepokea kwa masikitiko makubwa kuhusiana na kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Dkt.John  Pombe Magufuli ambapo amesema ni pigo kubwa kwa Watanzania kwani alikuwa shupavu  na mpambanaji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 18,2021 Spika Ndugai amesema Hayati Magufuli wakati wa uhai wake mambo  mengi  amesimamia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu mbalimbali na Rais ni sehemu ya mhimili wa pili wa Bunge hivyo kamati zote za bunge zilizokuwa zimetawanyika katika ziara za kukagua maendeleo zimesitisha  .

Sauti ya Spika Ndugai

Aidha,Spika Ndugai amesema hotuba mbalimbali alizotoa Dkt.Magufuli zitaendelea kusimamiwa kwa manufaa ya watanzania  .

Wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya chemba ambae pia ni Diwani wa Kata ya Mondo Saidi Sambala  amesema Hayati Dkt.John Pombe Magufuli  alikuwa mpenda watu na amewasaidia sana Watanzania kuzijua haki zao huku akisema watamkumbuka sana kwa mengi.

 INSERT….. SAMBALA  

Sauti ya Saidi Sambala Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Chemba

kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma na Mwenyekiti wa Taasisi za Elimu ya juu Tanzania Dkt Paul Loisulie amesema Hayati Rais Dkt John Magufuli  enzi akiwa waziri wa ujenzi alikuwa ni mtu aliyependa kulisimamia jambo lake na kuhakikisha linakwenda kwa weledi hadi kukamilika kwake .

Sauti ya Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma na Mwenyekiti wa Taasisi za Elimu ya juu Tanzania Dkt Paul Loisulie

Hata hivyo JFIVE TV.COM imezunguka katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dodoma hususan sehemu za machinga na kuzungumza na mama mmoja ambaye hakutaka jina lake kutajwa amesema Rais Magufuli alikuwa mtu wa kujali machinga hali  iliyosababishwa mama huyo ashindwe kujizuia na kuangua kilio.

Sauti ya Mwananchi
Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »