WAANDISHI WA HABARI WAMETAKIWA KUWA WAZALENDO KWA NCHI YAO NA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

WAANDISHI WA HABARI WAMETAKIWA KUWA WAZALENDO KWA NCHI YAO NA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

IKIWA leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari  Duniani baadhi ya Wadau  mbalimbali wa Habari wametoa maoni yao kuhusiana na siku hii huku wakitoa  pongezi kwa waandishi wa habari kutokana na kazi ambazo wamekuwa wakifanya katika  kuhabarisha Umma na kutoa wito  kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kuwa wazalendo  kwa kutanguliza mbele maslahi 

Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Innocent Bashungwa .


IKIWA leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari  Duniani baadhi ya Wadau  mbalimbali wa Habari wametoa maoni yao kuhusiana na siku hii huku wakitoa  pongezi kwa waandishi wa habari kutokana na kazi ambazo wamekuwa wakifanya katika  kuhabarisha Umma na kutoa wito  kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kuwa wazalendo  kwa kutanguliza mbele maslahi  ya  Nchi yao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Jfive hii leo  wamesema kuwa Siku hii ni muhimu kwa Wandishi wa habari hivyo ni mambo mengi yanajadiliwa na Waandishi wa Habari kwa lengo la  kusaidia kuboresha vyombo vya habari na utendaji kazi wa waandishi wa Habari.

Mmoja wa Wadau hao ni Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwipopo amesema waandishi ndio kiunganishi cha wananchi na Serikali ni vyema kuwa wazalendo huku Mthibiti  Mkuu Ubora  wa Shule Wilaya ya  Mpwapwa amesema Serikali imekuwa ikitoa nafasi kwa waandishi wa habari licha yakuwepo kwa changamoto mbalimbali  huku akitaka kupunguzwa kwa adhabu kwa vyombo vya habari ambavyo vinafungiwa kutokana na kukiuka Sheria pamoja na ugumu wa upataji wa habari kwa waandishi Serikali iangalie hilo.

Naye Afisa Elimu kata ya Chamkoroma wilayani Kongwa Sifrasi Japhet Nyakupola amesema Serikali ivipe uhuru Vyombo vya Habari kufanya kazi katika kuibua masuala mbalimbali na mambo hayo yasifichwe katika kujenga uelewa wa pamoja   ili kufikia uchumi wa kati .

Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwipopo na Afisa Elimu kata ya Chamkoroma wilayani Kongwa Sifrasi Japhet Nyakupola.

Hata hivyo  baadhi ya Waandishi wa habari nao walikuwa na haya yakusema.

Wanahabari

Na. barnabas kisengi

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Translate »