MWENYEKITI KANISA SDA JIMBO LA KUSINI MWA TANZANIA MCH.MARK WALWA MALEKANA ATOA WITO KWA VIJANA KUFANYA KAZI KWA BIDII NA KUACHA UTEGEMEZI KWA WAZAZI

MWENYEKITI KANISA SDA JIMBO LA KUSINI MWA TANZANIA MCH.MARK WALWA MALEKANA ATOA WITO KWA VIJANA KUFANYA KAZI KWA BIDII NA KUACHA UTEGEMEZI KWA WAZAZI

Na Barnabas Kisengi-Dodoma  Mwenyekiti kanisa la Waadventista Wasabato jimbo la kusini Mwa Tanzania Mch. Mark Walwa  Malekana  ametoa wito kwa vijana kuwa na mpango mkakati wa  wa kufanya kazi  kwa bidii ili kujikwamua kiuchumi na kuachana na dhana ya utegemezi kutoka kwa wazazi. Mchungaji Malekana amebainisha hayo  leo Juni,12,2021 katika mwendelezo wa mkutano wa shangwe

Na Barnabas Kisengi-Dodoma 

Mwenyekiti kanisa la Waadventista Wasabato jimbo la kusini Mwa Tanzania Mch. Mark Walwa  Malekana  ametoa wito kwa vijana kuwa na mpango mkakati wa  wa kufanya kazi  kwa bidii ili kujikwamua kiuchumi na kuachana na dhana ya utegemezi kutoka kwa wazazi.

Mchungaji Malekana amebainisha hayo  leo Juni,12,2021 katika mwendelezo wa mkutano wa shangwe katika njia Yake ,Kizota Net,Event,2021 ambapo amesema pamekuwepo na kasumba kwa baadhi ya vijana kuwa  na uvivu na kutegemea kwa wazazi ambao ni wazee hivyo ni wakati sasa umefika kwa vijana kufanya kazi kwa bidii.

Aidha,Mchungaji Malekana ametoa hamasa kwa kwa vijana na watanzania kwa ujumla kuacha anasa  na kujikita zaidi kufanya  mambo yampendezayo Mungu  pamoja na  kuhimiza uvaaji wa  nguo    za maadili .

Kuhusu suala la uimbaji kanisani,Mchungaji Malekana ametoa wito kwa kwaya zilizo ndani ya kanisa la Waadventista Wasabato kuimba kwa  kufuata kanuni za uimbaji ndani ya kanisa   huku akitumia fursa hiyo kuipongeza kwaya ya  Sauti Jangwani kutoka Mkoani Shinyanga kwa kuelendelea na uimbaji mzuri  huku pia  akiwaasa vijana waliopotea kwa kujikita katika dawa za kulevya,uasherati kurejea kwa Yesu Kristo kwani yeye ndie Mwokozi wa kweli.

Katika Sabato ya leo Juni 12,2021 Jumla ya watu 47  wamebatizwa kwa maji mengi baada ya kukiri na kumwamini Yesu kristo kuwa mwokozi katika maisha yao ambapo wamesema kanisa la Waadventista Wasabato ulimwenguni linasimamia misingi bora na ukweli kuhusu biblia ndio kivutio kiuu kwa kubatizwa .

Jfive Team
ADMINISTRATOR
PROFILE

Posts Carousel

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked with *

Latest Posts

Top Authors

Most Commented

Featured Videos

Translate »